Wanajeshi 8 Wahukumiwa Kunyongwa Baada ya Kukimbia Maadui Vitani...

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Wanajeshi wanane, wakiwemo maafisa watano, wamehukumiwa kifo kwa uoga na kuwakimbia maadui na Mahakama ya Kijeshi huko Goma, Mashariki mwa nchi.

Hukumu hii ni ya kwanza tangu kuondolewa kwa kusitishwa kwa adhabu ya kifo nchini DRC. Askari watatu waliachiliwa huru ambapo wote walikuwa wamepelekwa Kivu Kaskazini katika kupambana na waasi wa M23.

Kulingana na Mwendesha Mashtaka, mnamo Desemba 24, wanajeshi hao walipelekwa karibu na Saké, takriban kilomita 20 Magharibi mwa Mji Mkuu wa mkoa wa Goma, katika mapigano yaliyowahusisha Jeshi la Congo, washirika wake na M23 wanaoungwa mkono na Rwanda na kisha wakawakimbia waasi, kwa mujibu wa Mahakama.

Mawakili na wateja wao sasa wana siku tano za kukata rufaa. Askari wengine watatu waliachiliwa huru.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad