DR.MWAKYEMBE AMCHANA LIVE MBUNGE VITI MAALUM CHADEMA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Juzi tulisikia mipasho ya Mbunge wa Viti Maaluma CHADEMA, Mariamu Msabaha, kuhusiana na matatizo ya Air Tanzania.
Tatizo kubwa la Mama Msabaha ni pengine hakujua anachokiongelea.

Lakini jana ilikuwa zamu ya Dr Harrison Mwakyembe, Waziri wa Uchukuzi, kurudisha mapigo yanayostahili.

Mwakyembe kwanza kaanza na kumtaka Mariamu Msabaha kutosema jambo ambalo halifahamu au hana uhakika nalo.
Mwakyembe alikuwa akijibu hoja ya mama Msabaha kuwa ndege ya Air Tanzania iendayo Burundi, ilikuwa "inavuja".

Mwakyembe alijibu kuwa ili ndege iruhusiwe kuruka angani ni lazima kupata vibali mbali mbali kutoka mashirika mbali mbali likiwemo la kiamataifa la usafiri wa anga (ICAO) na lazima ikidhi viwango.


Mwakyembe alisema....
"Mheshimiwa Naibu Spika inashangaza kuona mbunge anakuja hapa na kudiriki kusema bila woga eti ndege inavuja,tena kimipasho tu 'ndege inavuja', hiyo inashangaza.


Mwakyembe aliendeea kumnanga mbunge huyo kuwa maneno hayo angeyasema Mheshimiwa Nd Omari Nundu, mbunge ambaye ana utaalam wa hali ya juu katika masuala ya ndege, basi asigeshangaa.

Lakini kwa hao wabunge ambao entry point zao bungeni ni kujua kusoma na kuandika tu ( Du F4F????) , anamsgangaa huyu Mariam Msabaha.

Mwakyembe aliendelea , endapo ndege hiyo ingekuwa inavuja isi ngeweza kuruka na kamwe (tatizo hilo lingekuwepo) isingeruhusiwa kuruka.

"Siyo mtu anainuka na kusema ndege hiyo inavuja huku hajui chochote juu ya usafiri wa anga, tena anajaribu kuwakataza hata watu kutumia ndege hiyo hapa Bungenini jambo la kusikitisha"

Du, hapo kuna mtu kaingia mlango si wake!!!
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Kaingilia mlango wa kutokea tuseme

    ReplyDelete
  2. Akome asiwe anabwatuka bila kuwa na evidence sijui wanatumwaa au vp halafu unadhalilika Umekomeshwaaaa

    ReplyDelete

Top Post Ad