HABARI MBAYA KWA WALA NGURUWE A.K.A KITIMOTO HII HAPA

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) kimehadharisha walaji wa nyama ya nguruwe nchini, kuwa wanakabiliwa na hatari ya kupata kifafa.

Utafiti wa kisayansi uliofanywa na SUA, umebaini kuwa baadhi ya nguruwe wana minyoo aina ya tegu ambao nyama yao ikiliwa bila kuiva vizuri, mlaji atapata minyoo hiyo ambayo huingia kichwani na kusababisha kifafa.

Akizungumza na mwandishi hivi karibuni, Mhadhiri na Mtafiti wa Idara ya Sayansi ya Wanyama na Uzalishaji ya SUA, Profesa Faustine Lekule, alisema sampuli za utafiti huo kutoka Mbeya, zimebaini nguruwe wengi wakiwamo wanaosafirishwa katika miji mikubwa wameathirika na minyoo hiyo.

Kwa mujibu wa Profesa Lekule, wataalamu wa SUA wanaosimamia Mradi wa Utafiti wa Kuboresha Ufugaji wa nguruwe kwa mkoa wa Mbeya ili kuinua pato la kaya, unaofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Denmark (DANIDA), walibaini hatari hiyo baada ya kuchukua sampuli ya nyama ya nguruwe kwa ajili ya vipimo.

“Majibu ya sampuli ambazo wataalamu wamezichukua kutoka kwa nguruwe wa wafugaji kwenye baadhi ya vijiji, wamebainika kukumbwa na hatari hii. 

“Lazima jitihada za makusudi zichukuliwe katika kutafuta ufumbuzi wa pamoja wa tatizo hili kati ya watafiti na Serikali,” alisema Profesa Lekule.

Alisema maambukizi ya tegu au minyoo ya nguruwe yanatokana na tabia za baadhi ya wafugaji kutozingatia ufugaji bora kwa kuwaacha kujitafutia chakula na maji mitaani na kula kinyesi cha binadamu.

Kwa mujibu wa Profesa Lekule, baadhi ya wafugaji wamekuwa wakijisaidia vichakani na kuwaacha nguruwe kutafuta malisho katika vichaka na kula kinyesi chao, hali inayochangia ongezeko la maambukizi ya minyoo ya tegu hao.

Baada ya kula kinyesi minyoo humwingia mwilini na kumdhoofisha na baadaye binadamu anapokula nyama ambayo haijaiva vizuri, minyoo hiyo humwingia na kusababisha kifafa baada ya kuingia kichwani.

Alisema athari za kuenea kwa maambuziki hayo inaweza kutokea katika miji mikubwa ikiwamo Dar es Salaam kwa kuwa nguruwe wa Mbeya husafirishwa na kuuzwa maeneo hayo.

“Hatua hii inaweza kusababisha kusambaa kwa ugonjwa huu, hivyo ushirikiano kati ya wafugaji, wafanyabiashara, Serikali na wataalamu wa afya katika kufikia hatua ya kumaliza changamoto hii unahitajika,” alibainisha Profesa Lekule
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

32 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Waendelee kula tu na upumbav wao na uroho wao

    ReplyDelete
    Replies
    1. We kuma tu acha watu wale kwn ww kinachokukera nn?

      Delete
    2. mpumbavu mwenyewe

      Delete
    3. Mungu alivyokataza mkamuona hana maana mtakoma

      Delete
    4. Mie nimesoma pia sua na huyo ni proffeso alienifundisha..sasa kwa taarifa yenu. hata ng'ombe wana minyoo wasipoiva vizuri wanaleta magonjwa. kwa hiyo msione mtu anakula pork akadunda wewe unaesema nini hapo ukafa kwa magonjwa mengine ya nyama ya ng'ombe.

      Delete
    5. Mnasema Mungu kakataza lakini mbona mwezi wa Ramadhani hii biashara inadororora?ndio kusema kwa kuwa watu wako kwenye mfungo hawana fursa ya kujiachia na mijiguruwe! Kama kufa tutakufa tu lakini siachi maana ni tamu kushinda nyama yoyote duniani.

      Delete
  2. Mi nakula kama kawa

    ReplyDelete
  3. Acheni usenge hilo suala tunalijua tangia chekechea au mmekosa cha kuandika

    ReplyDelete
  4. Kwa raha zetu mbona haram nyingine mmezipitisha kama suna mnaloooo wadau wenzetu nyie

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hahahahaha ,Anoy 3:11 ,Nimekupenda

      Delete
  5. Hata ikileta ugonjwa gani siwezi acha kula!!!! Bora uninyime kuku kitimoto we niachie!!

    ReplyDelete
  6. wataliwa tuuu wewe kinachokuuma nini mjinga wewe!

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ajabu! pilipili ziko shamba zinawashaje? Ni waongo mbona tunakula nao.

      Delete
  7. haramu iliyopitishwa kuwa suna ni ipi? nguruwe mwitu we kasoro mkia, makalio meusi kama chungu kilichopikiwa kuni kwa kula nguruwe, kitabu gani cha dini kimekuambia ule nguruwe? uroho tu, wabishi kama

    ReplyDelete
  8. hahahaha apana chezea kiti moto asiyekula atajiju nyiye tungeni siye twajilia ata sasa niko apa naagiza

    ReplyDelete
  9. Hicho kifafa hadi leo x ngeshakufa, uzushi mtupu

    ReplyDelete
  10. Wote mnaoponda nguruwe nimikundu tena mnapigwa miti ya nyuma na mtuache tuleee ......

    ReplyDelete
  11. Aliyekuambia nguruwe kakatazw nani? Bwege wewe! Usisome biblia kiislam, na wala usisome msitari mmoja basi, tambua kuwa najisi inatoka moyoni, mbona mengi mmekatazwa hamyasemi? Sie kwetu tangu watoto tunakula nguruwe, hadi mababu zetu wamefariki hawajawai kupata hicho kifafa, masharti ya nyama yoyote ile yanazingatiwa kuwa nyama lazima iive vizuri, alivyo mtamu tumuachie nani? We unafikiri tisipowala wataenda wapi? Na mbadala wake hakuna, acheni kitimoto iitwe ktimoto.

    ReplyDelete
  12. we adm unapota post uwe unatumia akili,

    ReplyDelete
  13. Mie siwez kuacha sie wazee wetu wamekula tangu wadogo mpaka sasa mbna hawajaugua.

    ReplyDelete
  14. Mpumbavu mamaako,mbona bangi mnavuta kwani hamjui madhara yake halafu leo ndio mnaanza kushoboka na kitimoto?tena ngoja niende zangu kumekucha nikajipigie NGURUWE nusu na valeur ndogo.......shwaiiin

    ReplyDelete
  15. Hao hao unawakuta Bar wanagonga bia za kufa mtu... Inamaana wanachagua dhambi... Nani kakataza kitimoto? Acheni hiyo mambo kabisa... Kitimoto lazima aliwe... Mtakuja kufa njaa na imani za ajabu ajabu.

    ReplyDelete
  16. Ngoja niende zangu kwa mama kamche saiv na kiroba nlale!!!!

    ReplyDelete
  17. Mbona dhambi mnachagu kuhua watu sio dhambi ila kitimoto ni dhambi kwa taharifa yako we pumbu waharabu wote hapa majuu wanategemea biashara ya nguruwe kuishi na nimeona yanakula sana

    ReplyDelete
  18. HII KWELI HABARI MBAYA

    ReplyDelete
  19. we naima peleka kisimi mbele uko umeona kula nguruwe haramu lakini kutiwa ovyo kabl ahujaolewa sio harama kajambe ukalale

    ReplyDelete
  20. ehh...kitimoto ya leo ni tamu jamani!!! uwiiiii ntavua nguo bureee

    ReplyDelete
  21. Uwiiiiii aitaiacha kamweeeeeeeee

    ReplyDelete
  22. kila kitu kina madhara!!sio hot chair peke yake,isitoshe haya maneno nimeanza kuyasikia toka mwaka 1986 hadi leo sijaona effect yake!!kuku,red meat,nyuchi sukari,chumvi etc vyote vina madhara!!

    ReplyDelete
  23. Kitu chochote kikizidi ni sumu

    ReplyDelete
  24. HII NYAMA NI TAMU SANA NA HAINA MADHARA

    ReplyDelete

Top Post Ad