MANENO YA LUKUVI YATIMIA CHADEMA NAYO IMEINGIA KATIKA MTEGO MZITO

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Hapa kuna ajenda za siri ukweli mchungu ni huu hapa na nitaendelea kuwaletea siku hadi siku hata kama ni mchungu lakini ndio dawa sasa. UKAWA sasa imeingia kwenye mtego mzito wa UAMSHO na upande wa pili kuna taarifa za siri mtoto wa Sultan wa Oman alikutana mara kwa mara na Sharif Hamad Uingereza kuhusu kuipa Zanzibar mamlaka kamili na ameapa kuisaidia kifedha na kimbinu na pia wameahidiwa mengine mengi, hapa ni pakuchunguza sana tena kiintelejensia haswa. 

Hapa sasa picha kamili inaonekana bila chenga kabisa hebu weka ushabiki pembeni alafu mtanielewa kwanza kumbukeni Lukuvi ni kiongozi wa juu kabisa wa serikali ukiachana na ujumbe wake ndani ya bunge maalumu la Katiba sasa kama ni taarifa za kiintelejensia atakua ameshazipata siku nyingi sana na ndio maana yeye kama mjumbe alitoa maoni yake kikamilifu na akaligusia hilo na kulifafanua bila uwoga kabisa maana hata ukimuuliza hana wasiwasi na anakuhambulia kimoja kimoja. 

Napata mashaka hapa ya kiusalama katika taifa hili changa kuna watu wana yao ila wanatumia UKAWA kama kivuli tuu cha kutetea wanyonge na tatizo jingine lililojitokeza ni hiki chama kikuu cha upinzani CHADEMA kujiunga na marafiki asiowajua kiundani sasa sina budi na yeye nimweke kundi hilohilo na ajenda hizohizo kwasababu wote ni UKAWA. 

Maswala madogo na marahisi ya kujiuliza ni haya hapa kwanini vuguvugu lao lianzie Zanzibar kule kwenye UAMSHO.? 

Je walipokua Zanzibar hawa viongozi wa UKAWA tuna uhakika gani kama hawakukutana na UAMSHO.? Maana hapa kuna shutuma za CUF kua na uhusiano na UAMSHO.

Shutuma alizozitoa Lukuvi zina ukweli wowote? Maana Lukuvi ana kofia mbili huyu ya uwaziri na ujumbe sasa kama ni taarifa za kiintelejensia atakua nazo tu bila shaka.

Wameshindwa plan A je plan B watafanyaje au watakua ni kikundi cha waasi.?

Kuhusu kurudi kwa Sultan wa Oman vipi wameshakutana na Sharif kujadili.? Pia kuna taarifa za chini kwa chini kua hata PEMBA na UNGUJA zinavuguvugu la kujitenga kila mmoja kivyake, hata Nyerere aliliona na alishalionya mapema kama naongopa nikosoe. Pia kuna kauli fulani za wanzanzibar bungeni kama "Ya wazanzibar tuachie wenyewe tunajuana" hii kauli ni pana sana na ina maana kubwa.

CHADEMA ameungana rafiki asiomjua kiajenda aachane nao haraka sana hapo ni WORKING TIME BOMB.

Ushauri wangu kikundi cha UKAWA kifutwe tu nina wasiwasi kitakua kikundi kamili cha waasi kwanza siyo rasmi na wakiendelea na hujuma zao wachukuliwe hatua kali kabisa na kiitwe rasmi ni kikundi cha waasi
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

21 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Wakamuulize Mapalala, CCW na KAMAHURU

    ReplyDelete
  2. Si zani kama wewe na lukuvi ni wazima,mnaona jambo la hatali siku nyingi hamsemi mnamaana gani?mnasema sababu wametoka bungeni wasinge toka mngeendelea kunyamaza acheni uchochezi tubaki na nchi yetu yenye amani.

    ReplyDelete
  3. Acheni usenge ccm mmeshaanza ufirauni we nu wa kutunga mambo siwapendi nyie

    ReplyDelete
  4. sultan wa oman.mbona haijulikani kama ana mtoto na watu wa oman wanasema hawajawahi kumuona wala kusikia mtoto wa qaabus.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hawa ni waongo tu mbona Qabus mwenyewe hajulikani kama ana mtoto? Wakati Qabus mwenyewe ndio Sultan wa Oman. Hapo kweli lazima utagundua uongo wao!

      Delete
  5. Huna uhakika na unachoabdika..ndio maana package kubwa ya maelezo yako imetawaliwa na dhana....huna jipya zaidi ya kukereketwa na kanisa....

    ReplyDelete
  6. A cha upumbavu kama huna lakusema kaa kimya.

    ReplyDelete
  7. Iko poa wachunguzwe

    ReplyDelete
  8. Just politics no big deal!

    ReplyDelete
  9. Wewe tupe burudani usiingilie hayo,wenzako wako kwenye ulaji ndio kazi yao,wewe ukiumwa utaenda Temeke wenzio Marekani!

    ReplyDelete
  10. siasa ndio inayoleta vita hapa duniani.

    ReplyDelete
  11. Hawa wanasiasa tukifanya mchezo watatupeleka mahali pabaya sana sisi wananchi tunatakiwatuwe makini sana tukiwaendekezs manenoyao mwishowake ni vurugu nszikitokea vurugu wote watakimbia watuachie msala cc wanyonge wote nafamilia zao weatakimbia tuwe makinijamani wacheni udjabiki.

    ReplyDelete
  12. tanzania ina matäbaka viongozi ndio wa kwanza kuleta udini na ubaguzi na viongozi wao dini wakifanya hivyo kundi lingine wachochezi, viongozi wanakosa busara na subira. Huwezi kutatua tatizo kwa kuanzisha tatizo lingine ambalo linaweza kuwa kubwa kuliko hilo la awali.

    ReplyDelete
  13. Kweli UKAWA wanataka kufanya ujinga

    ReplyDelete
    Replies
    1. hapo wananchi ndo muamke na mjue wako kwa ajili ya maslah yao, unless othewise wangepigania katiba hii mpya kwa maridhiano na kushinda kwa hoja, washaona hawana hoja za kuwaconvece wananchi na bunge ili wakubaliane nao, lkn ukweli kamioli wanao nyuma ya pazia hapo ndo pagumu, ndo mjue ni wanafki na hawaitakii jema taifa hili na siku zote mungu hamfichi mnafi

      Delete
  14. Kama wamekutana Uingereza lazima ushahidi utapatikana ataje tu mtaa au hoteli au popote walipokutana ushahidi utatoka live,labda iwe miaka 20 iliyopita lakini kama ni miaka mpaka 10 iliyopita data zote zitakuwepo!

    ReplyDelete
  15. kweli ukisikia watu kukosa maneno ndio huku, mtu unapoteza muda kuandika pumba hizi au unaandikia matako? Ukawa ukawa,,,,

    ReplyDelete
  16. Huyu Muandishi Msenge kweli hivyo katika karne hii ya 21 bado analeta mambo ya Usultan kurudi Zanzibar....Hebu tuwachieni Sultan Qaboos wetu, ya 1964 inatosha wacha tule matunda yetu ya Oman hakuna siasa chafu.

    ReplyDelete
  17. mohamed merickzedeck22 April 2014 at 12:32

    Chadema kama chama makini na kimejipambanua hivyo hakiwezi kikawa na permanent ENEMY au Permanent FRIEND.so ukijalibu kukihukum kwa muungano huu wa UKAWA utakua unafanya makosa kwa sababu chadema na Cuf vyote n vyama vya upinzani hivyo kuna agenda ambazo km vyama makini lazima visimame kwa pamoja,hofu itakua ni kwenu ma-CCM maana muungano huu kwenu ni hatari tupu zidi ya utawala wenu,halafu kitu kingine hii nchi ni kwamba haijawahi kua na taarifa za kweli za kiintelijensia kama inavyohubiliwa ila ni ubabaishaji na hapo ndipo ccm hua inapata ahueni inaposaidiwa na vyombo husika pale inapobanwa mbavu.kwa hiyo Lukuvi kadanganya tena si kwa bahati mbaya ila kimkakati,sasa usiandike mada zako za kutetea hata visivyohitaji kutetewa.

    ReplyDelete

Top Post Ad