Jaji Werema Adaiwa Kumtishia kifo Kafulila Bungeni Dodoma

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwanasheria mkuu wa serikali jaji Fredrick Werema ametuhumiwa kumtishia kifo mbunge wa Kigoma Kusini mh David Kafulila,Imedaiwa kuwa jaji Werema alimtolea maneno hayo ya vitisho mh Kafulila jana asubuhi kwenye viunga vya bunge mjini Dodoma baada ya bunge kuahirishwa.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii,mh Werema alimtolea maneno hayo ya kitisho mbele ya mwenyekiti wa Bunge Mussa Hassan Zungu,mwandishi wa habari mmoja alietajwa kwa jina moja la Butare,akiwa na waandishi wa habari wenzake ambao hawakutajwa majina yao ,wakiambatana na mpiga picha ambaye pia ametajwa kwa jina la moja la Edwin na baadhi ya wabunge kadhaa waliokuwa wanapita,mh Werema amanukuliwa akimwambia mh kafulila kwamba "I will take your head,unless you apologize"ikimaanisha atamkata kichwa iwapo hatamwomba msamaha,

Kufuatia sakata hilo mh Kafulila amemthibitishia ukweli wa madai hayo mwandishi wa Bloghii ya " http://nicholauskilunga.blogspot.com/" na kwamba tayari ameshachukua hatua kwa kuiandikia barua ya madai ya kutishiwa maisha ofisi ya spika wa bunge,huku nakala ya barua hiyo akiipeleka kwa mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Mangu na nakala nyingine ameipeleka kwa kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma(RPC Dodoma)mh Kafulila aliendelea kuongea na mwandishi wa habari hii akisema"ni kweli nimetishiwa maisha na mwanasheria mkuu wa serikali leo asubuhi kwenye viunga vya bunge,na nimekwisha chukua hatua tayari,lakini watanzania wakumbuke kwamba nilipokuwa nikichangia hoja ya ufisadi huu wa Escrow wakati wa bajeti ya wizara ya nishati,nilisema,hata kifo cha Mgimwa kilipaswa kuchunguzwa, kwasababu aliugua na kufariki kipindi ambacho kulikuwa na pressure kubwa ya kuzitoa pesa hizi za Escrow na hivyo kuna mashaka sana kuhusu kifo cha waziri huyo hasa ikizingatiwa makosa yaliyofanywa na Hazina na BOT kwa kushirikiana na wizara ya nishati na madini na jaji Werema alihakikisha hizo Bilioni 200 zinatolewa"alimaliza kuongea mh Kafulila.

Mbunge Kafulila ambaye pia ni mbunge Kigoma kusini kupitia chama cha NCCR na waziri kivuli wa wizara ya Viwanda na Biashara,aliendelea kumweleza mwandishi wa habari hii kwamba jaji Werema anajua kila kitu kilichotokea kwenye mchakato huo,anasema jaji Werema ndiye aliyetoa ushauri wa kisheria na kuelekeza bank kuu kuruhusu utolewaji wa fedha hiyo na aliruhusu hayo akiwa kama mwansheria wa mkuu wa serikali,na hatua yake yake hiyo ya kuruhusu utolewaji wa fedha hiyo kufuatia wizara ya nishati na madini kuwa tayari ilikwisha saini makubaliano na kampuni aliyoiita ya kitapeli inayomilikiwa na mtu alieitwa na mh Kafulila kuwa Singasinga ijulikanayo kama PAP iliyopewa fedha hizo kama mmiliki halali wa wa fedha hizo wakti haikuwa na sifa hiyo.

Nae mh Werema alipopigiwa simu na mwandishi wetu na kutakiwa kuthibitisha ukweli wa taarifa hizi za madai ya kutishia kumwua mh Kafulila alijibu"Hilo jambo si jambo la kitaifa,tafadharini sana msilifanye kuwa la kitaifa,mimi nilifikiri umenipigia kwa ajili ya kuzungumzia mambo ya kitaifa,kwa hili sina majibu naomba uniache nipumzike"alimaliza kuongea mh Werema huku akikwepa swali la msingi alilokuwa ameulizwa na mwandishi hii,

Sakata hili liliibuka jana bungeni mjini Dodoma,kufuatia mwongozo uliokuwa umeomba na mh Kafulila kuhusiana na majibu ya waziri wa nishati na madini aliedai kwamba alilidanganya Bunge na kusema uwongo ndani ya bunge tena mbele ya waziri mkuu,pale alipokuwa akijibu hoja juu ya madai ya ufisadi kwenye akaunti ya Escrow na kusema kwamba fedha hizo zilitolewa baada ya kesi kuamuliwa,ndipo alipotaka muongozo katika suala hilo hali iliyomlazimisha mwanasheria wa serikali jaji Werema kuingilia kati na kujibu swala hilo kwa kusema taratibu zote zilifuatwa wakati wa utolewaji wa fedha hizo, na ni kweli kesi ilikuwa imekwisha amuliwa,wakati akiendela kuongea mh Werema alienda mbali zaidi kwa kulitolea mfano wa kabila lake kwamba wanamsemo mmoja kwamba Tumbili hana maamuzi ndani ya msitu hali iliyotafsiriwa kumlenga Kafulila ambaye nae alimjibu kwamba ni mwizi hali iliyompandisha hasira zaidi jaji Werema huku akivuka mstari na kutaka kwenda kumpiga mh Kafulila kabla wabunge kumzuia jaji Werema na baadae kutolewa nje na askari wa bunge.


Mheshimiwa Kafulila alisema kinachofanywa na serikali ni sawa na kile kilichotokea mwanzoni mwa miaka ya 2006 na 2007 pale katibu mkuu wa CHADEMA na aliekuwa mbunge wa jimbo la Karatu Dr Wilbroad Slaa pale alipoibua ufisadi mkubwa kwenye akaunti ya madeni ya nje yaani EPA,alisema mwanzoni mwa sakata lile serikali na chama cha mapinduzi walilipinga sana na kusema madai yale yalikuwa ya uzushi mtupu na kwamba hayana ukweli wowote,lakini baadae yalibainika kuwa madai ya kweli,

Tulijaribui kuwasiliana na ofisi ya spika kuthibitisha madai ya kupokea barua hiyo,lakini ilishindikana mpaka tunakwenda mtamboni,lakini tunawaahidi wasomaji wetu wapendwa kwamba kesho tutaweka hapa nakala ya barua hiyo,hivyo endelea kutusoma na kutufuatilia.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

6 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. hili bunge sasa halina hata mvuto wa kusikiliza wala kutazama, yaani wabunge ni kukashfiana, kutukanana,kusemana vibaya, sidhani kama ndio demokrasia inavyosema,
    mnatuchosha jamani angalieni msije mkaanza kuuana wenyewe kwa wenyewe mtamalizana, nakosa hata hamu ya kuwa kiongozi maana kama mambo yenyewe ndio hivyo sitaweza,
    mwisho wa siku mtaanza kutukana na wake/waume zenu huko bungeni
    mtaanza kwanza mke wa fulani sura kama mwajuma ndala ndefu,shape hana, ndiko mnaoelekea sasa
    sie yetu macho nyie chukueni tu hizo kodi zetu tutakutana majimboni msimu ujao

    ReplyDelete
  2. hakuna haja ya jaziba hapo nikujibu hoja tu msikimbie maswali mkaanza hadithi za ngedere jamani tunawasikiliza huku majimboni

    ReplyDelete
  3. Wizi wa mali ya uma ndio umewajaa viongozi wa ccm hakuna kingine hapo !jaji mzima unamtishia mtu maisha kweli?hmjazba yote hii ni kuambiwa ukweli kuma nyoko wewe mwizi mkubwa wa mali zetu!unafikiri utamuua kama ulivyomuua Mgimwa?fanya uone nguvu ya umma kuma nyoko zako!nyinyi mna jeshi la polisi sisi tuna nguvu ya uma tuone sasa!viongozi wa ccm ni wezi wakubwa na wameshatuona kuea watanzania ni mamburula ndio maana wako huru kujifanyia chochote kile Rais hawezi kuongea chochote kwanza sasa tunavyoongea yuko nje anakula bata!halafu kwa kashfa kama hizi za wazi wazi unakuta kunamijitu inashabikia chama cha majambazi kweli hivi watanzania huwa tumerogwa na nani?!

    ReplyDelete
  4. tena aliyeturoga kafa..................hii ni kweli kabisaaaaa

    ReplyDelete
  5. KWENYE HAKI HAKUNA HASIRA NA VITISHO !

    ReplyDelete
  6. Vibaka wakubwa.

    ReplyDelete

Top Post Ad