Polisi 'Mbasha Jitokeze Mwenyewe Kabla Hatujakutafuta Ulikojificha'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

TAHADHARI! Wakati akiwa hajulikani alipo huku akishtakiwa kwa tuhuma ya ubakaji wa shemejiye, jeshi la polisi Bongo limemtaka mume wa mwimbaji wa Injili, Flora Mbasha, Emmanuel Mbasha kujisalimisha mwenyewe.
Habari za ndani zilieleza kuwa polisi wa Kituo cha Tabata-Shule, Dar ndiyo wamemtaka kujisalimisha baada ya binti anayedaiwa kubakwa kufungua jalada kituoni hapo lenye namba TBT/RB/3191/2014 na ya Jalada la Uchunguzi namba TBT/IR/1865/2014 akidai kutendewa unyama huo kwa siku mbili (Ijumaa na Jumapili wiki mbili zilizopita).

Kwa mujibu wa chanzo makini kilicho ndani ya jeshi hilo, zoezi la kumsaka limeanza tangu Mei 19, mwaka huu aliposhitakiwa na shemejiye kituoni hapo lakini hadi gazeti hili linakwenda mitamboni Jumamosi jioni, jitihada zilikuwa hazijazaa matunda.

Ilisemekana kwamba licha ya kuweka mikakati kabambe ya kumtia nguvuni ili ahojiwe kuhusiana na tuhuma hizo huku jeshi hilo likimtaka Mbasha kujitokeza kabla nguvu nyingi hazijatumika.

“Tunamtaka ajitokeze mwenyewe kabla hatujatumia nguvu nyingi kumsaka, maana jeshi lina mkono mrefu hivyo hana ujanja na ukizingatia yeye ni mtu maarufu,” kilisema chanzo.

Ilidaiwa kuwa, Mbasha alitoweka nyumbani kwake, Tabata-Kimanga wakati ambao mkewe (Flora) alikuwa amehamia hotelini kutokana na ugomvi mzito waliokuwanao.

Taarifa zaidi zilisema, kwa kuwa mlalamikaji alifikisha malalamiko hayo polisi akiwa na viambatanisho vya vipimo vya daktari vilivyoonesha kuingiliwa kimwili kwa nguvu, Mbasha anatakiwa ajitokeze ili kutoa maelezo ya upande wake na taratibu za kisheria ziendelee.

Jitihada za kumpata Mbasha zilishindikana kwa kuwa simu yake haipo hewani kwa siku kadhaa sasa.
GPL
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad