AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Taarifa hizo zilieleza kuwa tukio hilo lilifanyika maeneo ya Mlimani City wakati Bob Junior alipokuwa akishuti vipande vya wimbo wake wa ‘Bolingo’ huku msichana huyo akijiachia mbele ya lens.
Ghafla mumewe akatokea na kuzua tafrani, video ya wimbo ikageuka kuwa ya ndondi na mwisho wa siku mwimbaji huyo alilazimika kukimbia kupisha shari.
Tovuti ya Udaku Specially imeongea na Bob Junior kuhusu tetesi hizo ambapo yeye amekiri kutokea kwa fujo hiyo lakini amekanusha kuhusu suala la kufanya video na msichana huyo ingawa alikuwa na directors wake na vifaa.
“Hapana, naona watu wanakuwa kama wambea. Mimi nilikuwa nimekaa pale Mlimani City tunapiga story niko na mwanamke wangu. Rafiki yangu mwingine alikuwa kaka na mwanamke mwingine, sasa sijui kama ni mke wa mtu au nini, ndio ikatokea vurugu lakini huyo mwanamke aliyefanyiwa vurugu mimi simfahamu.” Ameeleza Bob Junior.
“Tulikuwa tumekaa tu tunaenjoy tunapiga story, tunakula…mimi sijui kama ni mwanamke wake au ni mke wake. Amemfanyia vurugu, amemvuta nywele. Wamezinguana kidogo lakini sifahamu kama ni mke wake au ni mchumba wake ila najua ni mtu ambaye ana uhusiano nae.” Ameongeza.
Akizungumzia kuhusu taarifa kuwa alitoka nduki na kumuacha rafiki yake akifanyiwa fujo, Bob ameeleza kuwa aliondoka kupisha shari na sio kukimbia kama ilivyotafsiriwa.
“Hapana siwezi kukimbia siwezi kukimbia. Tanzania ni nchi yenye amani kwa nini nikimbie kuna vita gani jamani hapo. Mimi nilichukua vitu vyangu na vijana wangu na team Sharobaro wangu, nikaondoka taratibu nikachukua gari langu nikaondoka. Unapoona mtafaruku hupaswi kukaa kuendelea kuangalia jambo. Unapaswa kupisha uliache jambo liendelee.”
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
you
ReplyDelete