Lady Jay Dee Adaiwa Kuopoa Ka Serengeti Boy , Picha Zanaswa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Na Musa Mateja
OHOOO! Siku chache baada ya ndoa ya Legendary wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ na mtangazaji mahiri nchini, Gardner Gabriel Habash ‘G Habash’ kudaiwa kuvunjika, gumzo limeibuka kufuatia kunaswa kwa picha za Jide na kijana mmoja (dogodogo) aliyetajwa kwa jina la Meddy Ahmed ‘Mtoto wa Vitoto’, Risasi Jumamosi linakupa kinaga ubaga

TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, Mtoto wa Vitoto huyo amekuwa na urafiki uliotukuka na Jide kwa muda mrefu kabla na baada ya mtafaruku wa ndoa ya Jide na mumewe Gardner hivyo kudaiwa kuwa ndiyo faraja ya mawazo ya mwanamuziki huyo hususan kipindi hiki cha changamoto ya mgogoro wa ndoa yake.

Chanzo hicho kilizidi kumwaga data kuwa, ukaribu wa Jide na bwa’mdogo huyo ulipitiliza kiasi cha watu wa karibu na staa huyo kuanza kuhisi huenda wana uhusiano usiofaa.
“Ukaribu wao ulipitiliza hadi kila mtu wa karibu na Jide akautilia shaka, isitoshe kama unavyojua, Jide si mtu wa kuweka mambo yake hadharani. Mbaya zaidi Jide amekuwa akimposti dogo huyo kwenye mitandao yake ya kijamii,” kilisema chanzo hicho


ADAI NI MARAFIKI
Huku akiashiria sauti ya kutojiamini, dogo huyo alisema yeye na Jide ni marafiki wakubwa katika mazingira ya kawaida, pia  ni shabiki wake kama walivyo wengine ila ishu ya picha mtu yeyote anaweza kupiga.

Kuhusu kuendesha gari linalodaiwa ni la Jide, dogo alisema hajawahi ila ameshapiga nalo picha na mtu yeyote anaweza kufanya hivyo kama ana uhusiano mzuri na mwanamuziki huyo.
“Jide ni rafiki yangu na mimi ni shabiki wake wa kawaida. Kwa hiyo hilo siyo tatizo lakini pia kuhusu gari mimi sijawahi kuendesha gari la Jide lakini nimewahi kupiga nalo picha kweli kama shabiki mwingine na hakuna shida, ila siyo wapenzi, ni marafiki tu,” alisema Mtoto wa Vitoto.
GPL
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. acheni kukuza mambo msiyokuwa na uhakika nayo na vyanzo vyenu uchwala,mtu akipiga picha basi mtu wake loooh mna haribu heshima ya social network

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hawa sio wa kukaribisha majumbani ni wambea sana,sijui wanasomea kwanza.
      udaku sio mtunge mambo,andikeni ambacho una uhakika nacho

      Delete
  2. Udaku wasenge sanaaaaa hamna jipya chini ya jua.

    ReplyDelete

Top Post Ad