Tofauti Kati ya Wanamuziki Diamond Platnumz na Ali Kiba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Moja ya mdau mkubwa wa muziki nchini na mmiliki wa G Records, studio iliyomtoa Alikiba, Guru Ramadhan aka DJ G-Lover, amezungumzia tofauti iliyopo kati ya Diamond na Alikiba aliyewahi kuwa chini yake.

Akizungumza na Vijimambo, Lover ambaye akiwa meneja wa Alikiba walitoa album mbili, amewaka bayana uwezo wa kila msanii na jinsi walivyojikuta kwenye biashara.

“Kwa kweli tofauti ukija kwenye masuala uimbaji, wengi wanaongelea hata katika mitandao tofauti tofauti kwamba Ali ana sauti nzuri na anaimba vizuri. Hata Diamond kuna wakati alikuwa anakiri kwamba angekuwa ana sauti kama ya Alikiba basi angefanya mambo makubwa zaidi,” amesema G. “Lakini unapokuja kibiashara Diamond huwa anazungumza kUwa yeye muziki wake anaufanya kibiashara na ndo maana ana team work kubwa ambayo inamsaidia yeye kujua ni kitu gani anatakiwa kufanya, kuna kitu gani anatakiwa kukifanya kwa upande wa muziki. Sasa kwa upande wa Ali kwa sasa hivi, kwa kipindi niko naye nilikuwa na team ambayo hata yeye alikuwa hajui mimi nipo na akina nani nyuma yangu. Alikuwa anajua kuwa yupo G, lakini nyuma yangu nilikuwa na watu takriban thelathini ambao ni team work ambayo ilikuwa inafanya kazi kwa Ali Kiba kujua ni kitu gani na kitu gani tunatakiwa tufanye ili afike na mpaka akafika hapo,” aliongeza.

“Diamond naYe anafanya vitu kama hivyo, unaweza kuona Diamond ana team ya watu watatu tu au wanNe ambao wanamsaidia, kwaHiyo utaona Diamond kuna watu kibao ambao amewapa ajira. Kwahiyo Diamond hawezi kuwaangusha watu ambao wapo nyuma yake ambao wamepata ajira kutoka kwake. Kwa mfano kuna utofauti mkubwa ambao Diamond amekuja nao ambao ukiangalia ni utaratibu uleule ambao nilikuwa nikiufanya kwa Ali. Kwahiyo sijui kuna utofauti gani kati ya manamament ya Diamond na ya Ali Kiba ya sasa hivi
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

13 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. yani naona alikiba kaamua kutafuta kik kwa guvu kama alishidwa kutima charce yake enzi za kina R kely kamwe atazidi kuyuba yuba tu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Anajifanya eti alikuwa likizo wapi ndugu yangu. Maisha hayasubiri mtu atoke likizo.

      Delete
  2. tafadhali naomba msimpe kiki ali k kumuweka na d......hao ni levo mbili tofauti yaaaani who ali k...........futa hiyo takataka naomba msirudie kumwandika na d.......

    ReplyDelete
  3. Ali kiba si mbunifu na sio mtu anayejituma kama Diamond lakini pia msisahau kila msanii ana wakat wake Ali kama angekuwa na akil kipindi cha project ya R Kelly angefika mbali sana ila sasa asitegemee atakuja mfikia D alipo

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kwa kweli namhurumia huyo kijana. Amejiua yeye mwenyewe wala asitafute visingizio vingine na akae akijua sasa hivi game ni ngumu.Sijui atafanya nini labda akomae kwelikweli na hiyo itakua ni bahati. Aliingia mkenge kwenda kuoa na kuzaa aliridhika mapema alifiria muda utakuwa unamsubiri.

      Delete
  4. Ali Kiba ni mzembe amelegealegea hivi. Anategemea vyombo vya habari na ma fans wake kumpromote wakati haiendi hivyo. Kijana fanya kazi ionekane na ndio promotion zitakuja zenyewe.

    ReplyDelete
  5. Fanyeni yenu basi mbona huyo kiba ametulia akafanya yake mtu hatakama simsemaji mnamchokonoa mpk aongee akiongea ooo hanalolote.km kafulia cjui Yuko down kimziki simumuache?mnamfwata wanini kutwa mumuhoji.kiba usizungumze tena lolote wanakutafuta useme wakukosoe.wapotezee.mungu ndio kilakitu pigakazi ukimtegemea mungu nakazi simziki tu zipo nyingi za pesa nihiari yako.

    ReplyDelete
  6. ona ktk pic hiyo domo kama msukule

    ReplyDelete
  7. kiba kashafulia ana jipya uyo mwezeke ana.miliki matuzo kibao yeye ana miliki mbili tu ajipange tena sana

    ReplyDelete
  8. Point nnayoiona hapo ni uchangamkaji.. wote ni wanamziki wazuri au huenda hata kweli kiba akawa yupo juu but kwenye maswala ya promo fomo level nyngne.. lait kama domo ndo angeimba na R kelly saa hiz nahis yupo cash money au hata ashafanya colabo na akina usher beibber na wakali wengine.. but kiba akalizika na nahic akili yake wkt wa ile collabo ilikua "bongo watanikoma".. acha beef fanya kazi ndo itakayoongea c mdomo wako kwenye media.. domo sasa hivi yupo juu humfikii

    ReplyDelete
  9. ukimfananisha ali kiba na diamondi ni sawa na kufananisha bajaji(kiba) na mercedes benz(dangote)

    ReplyDelete
  10. Mmh! Mimi mbona kama sijaelewa kilichozungumzwa hapo juu......, naomba ufafanuzi kidogo.

    ReplyDelete

Top Post Ad