AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Hivi sasa Rais yupo katika mapumziko ya Sikukuu za Krismasi inayosherehekewa Desemba 25 kila mwaka na Mwaka Mpya itakayofanyika Januari Mosi.
Akizungumza na wazee wa Dar es Salaam Desemba 22 mwaka huu, Rais Kikwete alisema amemweka kiporo waziri huyo hadi atakapopata ufafanuzi wa mambo kadhaa na kwamba atakapojilidhisha ataujulisha umma.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue aliliambia gazeti hili jana kuwa Rais Kikwete bado hajakamilisha kulishughulikia suala hilo na kwamba litakapokuwa tayari wananchi watajulishwa hatua alizozichukua.
“Unakumbuka Rais alichosema? Bado analifanyia kazi, atakapomaliza tu mtajulishwa, sasa hivi ni kipindi cha sikukuu,” alisema Sefue.
Profesa Muhongo
Hata hivyo, Profesa Muhongo alipotakiwa kuzungumzia shinikizo linalotolewa la kutaka ajiuzulu kabla ya Rais Kikwete kutoa uamuzi wake, aliliambia gazeti hili jana kwa simu kuwa; “Mimi sasa sitaki kuzungumza na waandishi, mambo yangu yote wapo watu ambao wanaweza kuyazungumzia.”
Hata hivyo, katika hotuba yake, Rais Kikwete aliagiza kuchukuliwa hatua kwa aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakimu Maswi ili kupisha uchunguzi wa tuhuma kuhusu ushiriki wake kwenye kashfa hiyo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK