Daktari: Moyo wa Mchezaji Okwi wa Simba Ulisimama Alipogongwa Kisogoni na Beki Aggrey Morris wa Azam FC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Sweetbert Lukonge na Ibrahimu Mussa
MOYO wa mshambuliaji Emmanuel Okwi ulisimama kwa sekunde kadhaa alipogongwa kisogoni na beki Aggrey Morris wa Azam FC.

Okwi aligongwa katika mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Azam FC iliyomalizika kwa sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, jana.Daktari wa Simba, Yassin Gembe, amesema moyo wa Okwi ulisimama kwa sekunde kadhaa kutokana na pigo la kisogoni karibu kabisa na ubongo katika eneo la Medullar Oblangata.

“Hakikuwa kitu kidogo, tulilazimika kufanya tiba ili kurudisha mapigo ya moyo wake kwa kuwa ulisimama kwa sekunde kadhaa. Aliumia na uliona akitoa mapovu. “Baada ya hapo, tuliona ni vema kumfikisha Muhimbili ambako vipimo vyote vimefanyika. Imeonekana hakuumia sana na ameruhusiwa.

“Lakini mimi nimeamua kumpumzisha kwa siku mbili ili kuangalia kama atakuwa katika hali gani maana mwanzo unaweza kuona yuko vizuri kumbe kuna tatizo. “Ikionekana anaendelea vizuri, basi ataanza mazoezi lakini atakuwa chini ya uangalizi wangu,” alisema Dk Gembe.

Mshambuliaji wa Simba, Dan Sserunkuma alitumia muda mwingi kumlaumu Morris kwamba alishiriki kumpiga Okwi kiwiko, hata hivyo, alikuwa akikanusha.Okwi alibebwa haraka na kutolewa uwanjani na baadaye kukimbizwa Muhimbili ikiwa ni baada ya kuzinduka.

Kugongwa huko kwa Okwi, jana jioni kulizua gumzo kwa mashabiki wa soka nchi hasa wa Simba ambao walikuwa wakipiga simu katika ofisi za gazeti hili wakidai mabeki wamekuwa wakatili kwa washambuliaji.
 Wengi walitolea mfano wa beki George Michael wa Ruvu Shooting kumkaba mshambuliaji Amissi Tambwe wa Yanga.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. wana simba tushirikiane kumuombea okwi

    ReplyDelete
    Replies
    1. Sio wanasimba tu jamani,
      Sema wote wenye roho safi tumuombee Okwi.

      Delete

Top Post Ad