Mapya ya Gwajima yazidi kuibuka Dar, Bastola iliyokamatwa Juzi Gwajima Anaimiliki Kihalali

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mfano wa Bastola iliyokutwa
MAPYA yamezidi kuibuka katika sakata la Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Joseph Gwajima, baada ya kuthibitika kwamba bastola iliyokamatwa katika harakati za kile kinachotajwa kutaka kumtorosha kutoka katika Hospitali ya TMJ, Dar es Salaam, ni mali yake.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema jana kuwa uchunguzi wa kina na wa kitaalam, sasa umethibitisha silaha hiyo inamilikiwa kihalali na Askofu Gwajima.

“Kuhusu risasi 17 za short gun ni kwamba Askofu Gwajima anamiliki bunduki aina ya short gun yenye namba 102837 ambayo inatumia risasi za aina ya hizo zilizokamatwa,” alisema Kamanda Kova.

Bastola hiyo ni moja ya vitu walivyokamatwa navyo wafuasi 15 wa Gwajima, wanaodaiwa kula njama za kutaka kumtorosha usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita.

My Take: Najiuliza tu kwa sauti je ? Wachungaji kumiliki silaha inaingia akilini? Nilitegemea wanategemea sana ulinzi wa Mungu 
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad