Wanne Kunyongwa Mpaka Kufa Kesi ya Mauaji ya Albino

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Watu wanne waliohukumiwa jana na Mahakama Kuu kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kuua albino, wameongeza idadi ya waliokwisha kutiwa hatiani ili wanyongwe kwa kosa hilo kufikia 17 nchini.

Idadi hiyo imeongezeka baada ya Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mwanza kuwatia hatiani watu wanne jana kwa mauaji ya mwanamke mwenye ulemavu wa ngozi yaliyofanyika mwaka 2008.

Kabla ya jana, watu 13 walihukumiwa kunyongwa hadi kufa kutokana na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi katika maeneo kadhaa ya Tanzania hususan mikoa ya Kanda ya Ziwa kutokana na imani za kishirikina.

HUKUMU YA JANA
Watu wanne akiwamo mume wa marehemu, walihukumiwa adhabu ya kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mlemavu wa ngozi, Zawadi Mangidu (22), mkazi wa Nyamalulu, Kata ya Kaseme, wilayani Geita.

Hukumu hiyo ilitolewa na Mahakama Kuu, Kanda ya Mwanza, huku ndugu wa waliohukumiwa adhabu hiyo ya kunyongwa hadi kufa ambao walikuwa miongoni mwa wakazi wengi wa mji huo waliofurika mahakamani hapo kushuhudia hukumu hiyo, wakiangua vilio.

Waliokumbwa na adhabu hiyo ni Masalu Kahindi (54), Ndahanya Lumola (42), Singu Nsiyantemi (49) na Nassor Said (47), mume wa marehemu Zawadi Mangindu.

Mahakama hiyo iliwahukumu watu hao ambao ni wakazi wa wilaya hiyo, baada ya kupatikana na hatia ya
kula njama na kushiriki kumuua kwa kukusudia mlemavu huyo wa ngozi.

UAMUZI WA JAJI
Akitoa hukumu hiyo, Jaji De-Mello, alisema amezingatia kwa makini na tahadhari kubwa katika kufikia uamzi huo baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na mashahidi 12 wa upande wa mashtaka na utetezi, kwamba washtakiwa walitenda kosa hilo bila kuwa na shaka yoyote.

Jaji De-Mello alisema katika hukumu zilizotangulia, pia zilibainisha kuwa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi yamekuwa yakitekelezwa na mtandao mkubwa na siyo rahisi kuubaini kirahisi.

Jaji De-Mello alielekeza kufikishwa mahakamani wanunuzi wa viungo vya watu wakiwamo wenye ulemavu wa ngozi na waganga wanaopiga ramli.

Jaji alisema kwamba wauaji pekee ndiyo wamekuwa wakifikishwa mahakamani dhidi ya vitendo hivyo vya kinyama.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Safi sana adhabu nimeipenda itakuwa fundishp kwa wengine

    ReplyDelete
  2. WANGENYONGWA HADHARANI MAGAIDI HAYO YASIO NA HURUMA

    ReplyDelete

Top Post Ad