AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Akiongea na East Afrika Radio Shilole alisema amejiandaa vizuri sana katika shoo ambayo anapaswa kuifanya nchini Marekani siku za karibuni, na alipoulizwa atawezaje kufanya shoo hiyo wakati akiwa amefungiwa na BASATA, Shilole alionekana kupaniki na kubadilika na kumwambia mtangazaji kuwa yeye hataki kuzungumzia suala la adhabu iliyotolewa na BASATA na kusema suala hilo anapaswa kuulizwa mwanasheria wake Albert Msando.
Hata hivyo kwa upande wa BASATA, Afisa Habari wa baraza hilo, Bw. Basyeibya amesema adhabu ya msanii huyo ipo palepale na wao wanaamini kwamba msanii Shilole anaitekeleza adhabu hiyo na
iwapo atakiuka adhabu hiyo watachukua hatua nyingine zaidi mbele.
"Adhabu ya Shilole iko wazi kwa maana ya kuzuiwa kufanya onyesho ndani na nje ya nchi utakumbuka kuwa kosa ambalo lilimfanya kufungiwa alilifanya nchini Ubelgiji kwa hiyo adhabu yake ipo pale pale haijatenguliwa hivyo hatakiwi kufanya onyesho lolote ndani au nje ya nchi, “alisema Bw. Basyeibya na kuongeza kuwa, “Kama anaweza kukiuka adhabu hiyo sisi Basata iwapo atakiuka adhabu hiyo tutachukua hatua zaidi dhidi yake"
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Mao kayega basata UKAWA, ,, pole kwa kuichukia CCM
ReplyDelete