Hatimaye Jaji AGUSTINO RAMADHAN Atoa ya Moyoni Kuhusu Kuhama CCM

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais wa Mahakama ya Afrika ya haki za binadamu, Jaji Agustino Ramadhani, amesema hajawahi kupatwa na wazimu wa kufikiria kuhama Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Aliyasema kuhusu taarifa zilizoenea kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, kwamba yeye na Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Gharib Bilal, wapo katika mipango ya kuhamia kambi ya upinzani. 

Jaji Ramadhani ambaye alikuwa mmoja kati ya makada 42 waliojitokeza kuchukua fomu za kuwania nafasi ya kugombea urais kwa tiketi ya CCM, jina lake lilikatwa na Kamati ya Maadili kabla ya kufikishwa mbele ya Kamati Kuu (CC) ya chama hicho. 

Jaji Ramadhani ambaye alikuwa kimya tangu mchakato huo umalizike, alisema taarifa hizo na yeye ameziona kwenye mitandao. 

Hizo taarifa hata mimi niliziona kwenye mitandao ya kijamii, kwamba mimi na Mh. Bilal tutazungumza na vyombo vya habari kutangaza kuhama chama na kwamba tutasindikizwa na mzee Warioba (Jaji Joseph Warioba), wanaoeneza hayo ni watu wasiyo na adabu, sijawahi kupatwa na wazimu wa kufikiria kuhama CCM, alisema. 
Alisema yanayoenezwa kwenye mitandao dhidi yake, kuhusiana na kuhama chama hayana ukweli wowote.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Top Post Ad