Wananchi Wafunga Barabara Baada ya Gari la Polisi Kugonga Wanafunzi wawili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wananchi wa eneo la Misugusugu Wilayani Kibaha Mkoani Pwani hii leo wamefunga barabara baada ya Wanafunzi wawili kugongwa na gari la Jeshi la Polisi na kupelekea kifo cha Mwanafunzi Mmoja

Akiongea na Mtandao huu, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani Jaffary Mohammed amesema baada ya tukio hilo Wanachi walifunga barabara kutokana na hasira ya tukio lakini jeshi la Polisi limetuliza hali na linamshikilia Dereva wa gari hilo kwa uchunguzi zaidi.

Kamanda Jaffary ameongeza kuwa katika tukio hilo Mwanafunzi aliejeruhiwa amelazwa katika hospitali ya Tumbi na mwili wa marehemu upo mochwari katika hosptali hiyo.

Aidha Jaffari ameongeza kuwa kwa sasa hali ya kiusalama imetulia baada ya jeshi la polisi kutuliza hali iliyojitokeza huku akiwataka wananchi kuacha kujichukulia sheria mikononi na badala yale wafuate sheria.

Katika hatua nyingine amewataka madereva wafate sheria za barabarani kwa kufuata alama zilizowekwa pamoja na kupunguza mwendo katika maeneo ya watu ili kuepusha ajali zinazoweza kuepukika.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Top Post Ad