AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kati ya majimbo kumi, saba yamenyakuliwa na wapinzani. Matatu tu ndiyo yako chini ya CCM. Kabla ya uchaguzi huu, Dar ilikuwa na majimbo saba. Wapinzani walikuwa na mawili tu. Mambo yamebadilika.
Hii inamaanisha kuwa Manispaa za Dar es Salaam zitaongozwa na wapinzani. Kwahiyo, ni kama kusema, Serikali ya Dar es Salaam itakuwa ni Serikali ya wapinzani. CCM imepokwa uongozi wake hapa Dar es Salaam. Ni jambo zito. Ni jambo la maumivu makali.
Hata vigogo wa nchi hii wanaendelea kuishi kwenye jimbo linaloongozwa na wapinzani: Kawe. Vyuo vikuu karibu vyote vya Dar es Salaam vipo Kinondoni yenye majimbo manne: Kinondoni, Kawe, Ubungo na Kibamba. Yote yamenyakuliwa na upinzani. Yaani, Dar es Salaam ipo chini ya utawala wa UKAWA.
Sauti iliyovuma kutoka Arusha hadi Mbeya; toka Mbeya hadi Mara; toka Mara sasa imetua Dar es Salaam. Yote yafanyike lakini hili la Dar linauma sana. Ndiyo maana hata mpambano wa Urais bado ni mbichi sana kwakuwa majimbo ya Dar es Salaam bado hayajatangazwa.
Kuna la kufanyika kichama mwaka 2020!
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Haijalishi Dar kashika nani tunataka wachapa kazi hata hao walio pigwa chini wa ccm walikuwa hawajibiki,,, hata wao wasipo wajibika wata pigwa chini vilevile tanzania sio Dar tu.
ReplyDeleteHuu ni mwanzo wa mageuzi makubwa tanzania. Kwa upinzani kuikamata miji ya dsm, arusha, mbeya, moshi na bukoba n.k. kwa katiba iliyopo ni muujiza wa kihistoria. Kwa bahati mbaya katiba iliyopo haitoi madaraka muafaka kuziwezesha serikali za mitaa kuleta maendeleo chanya. Bado yamehodhiwa na serikali kuu na wateule wa Rais k.m. wakuu wa mikoa na wilaya! Usishangae kuona kijana kama Makonda ambaye hakuchaguliwa na wakazi wa Kinondoni akiwakwaza madiwani kutokana na ukada wake wa CCM! Haya ndiyo mapambano yaliyoko mbele yetu - kuwapa wananchi nchi madaraka ya kuamua maendeleo yao kupitia viongozi waliowachagua.
ReplyDeleteMagufuli Chonde Chonde
ReplyDeleteUkimchaguwa Nauye kuwa waziri utapata laana ya wana ntwara
Poleni kuchagua magufuli kwa Bao kona
ReplyDeleteUchaguzi si halali Kwani zanzibar ushafutwa
Makonda si mkuu WA wilaya tena
ReplyDeleteStands kurithi cheo mropokaji mwenzie.nape huko CCM
Shehe yahaya alitabiri haya
ReplyDeleteMwanga mkubwa tapeli mganga WA CCM