AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli, amesema kugundulika kwa gesi ya Bagamoyo mkoani Pwani itasaidia kuimarisha uchumi na ujenzi wa viwanda nchini.
Hayo aliyasema jana wilayani Bagamoyo katika mikutano yake ya kampeni iliyofanyika katika majimbo ya Chalinze na Bagamoyo, ambapo alisema gesi hiyo itasaidia ujenzi wa viwanda katika serikali yake.
"Kwanza niwapongeze kwa kugundua gesi hapa Bagamoyo, tena imegunduliwa katika eneo la ruvu. Na hii itakuwa na manufaa kwa uchumi wa Taifa na kwa wananchi wa Pwani kwa ujumla.
"Gesi hii itasaidia sana ujenzi wa viwanda vya kisasa katika serikali ya Magufuli ya awamu ya tano. Tutajenga viwanda na tutatoa ajira za uhakika kwa vijana wa nchi hii pamoja na Tanzania yote," alisema Dk. Magufuli
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwanadi wagombea ubunge wa jimbo la Bagamoyo Dk. Shukuru Kawambwa (kushoto) na jimbo la Chalinze Ndugu Ridhiwani Kikwete kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya Msingi Majengo,Bagamoyo.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Bagamoyo Dk. Shukuru Kawambwa mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya Msingi Majengo,Bagamoyo.
Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akimnadi mgombea ubunge wa jimbo jimbo la Chalinze Ndugu Ridhiwani Kikwete kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya Msingi Majengo,Bagamoyo.
Mgombea ubunge wa jimbo jimbo la Chalinze Ndugu Ridhiwani Kikwete akimnadi mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya Msingi Majengo,Bagamoyo.
Source:Mpekuzi Huru
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Bagamoyo kuna gesi
ReplyDeleteTutawakoma wakwele