Meseji Kutoka Jamii Forums Baada ya Kuvamiwa na Website yao Kutopatikana Jana Masaa 7

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Tunafarijika kuwafahamisha kuwa tumerejea hewani baada ya kupata mashambulizi ya makusudi yenye kulenga kuzuia upatikanaji wa huduma kwa watumiaji wa JamiiForums (DDOS Attack) kwa takribani masaa 7, kuanzia saa 7 mchana hadi saa 2 usiku.

Mashambulizi haya yaliyolenga kuidhoofisha miundombinu yetu, yamefanywa kwa kupangwa na kwa kiwango tulichobaini kuwa yalifanywa na wataalamu waliobobea katika masuala ya mashambulizi ya kimtandao.

Tunalaani kwa nguvu zetu zote kitendo hiki na vingine vya mwelekeo kama huu vyenye kulenga kunyamazisha sauti za wananchi.

Timu yetu ya wataalamu itaendelea kufanya kazi kwa umakini zaidi katika kipindi hiki cha Uchaguzi na tunaomba ushirikiano wa wanachama na wadau wa JamiiForums pale mtakapoona huduma zetu zinasuasua kwa namna yoyote ile katika upatikanaji. Wasiliana nasi kupitia support@jamiiforums.com

Tunawashukuru sana kwa uvumilivu wenu katika kipindi hiki na tunawatakia kila la heri katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu.

Maxence M. Melo,
K.n.y Uongozi wa JamiiForums
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Top Post Ad