AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Bodi ya TPA ilivunjwa Desemba 7 baada ya kugundulika kuwa zaidi ya makontena 2,670 yalipita Bandari ya Dar es Salaam bila kulipiwa kodi, hivyo kuikosesha Serikali mapato yake.
Kutokana na uzembe huyo, Rais aliivunja na kutengua uteuzi wa mwenyekiti wake, Profesa Joseph Msambichaka na katibu mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dk Shaaban Mwinjaka huku mkurugenzi mkuu wa TPA, Awadh Massawe akisimamishwa kazi.
Licha ya Mgassa kuwa mjumbe wa bodi hiyo, pia alikuwa meneja wa idara ya manunuzi ya UDSM.
Alipotafutwa kuzungunzia sakata hilo, kwa ufupi Mgassa alisema: “Samahani, siwezi kulizungumzia hilo.”
Makamu Mkuu wa UDSM, Profesa Rwekaza Mukandala alithibitisha kuenguliwa kwa mjumbe huyo. “Ni mabadiliko ya kawaida ambayo yanalenga kuimarisha utendaji uliotukuka wa chuo kikuu hicho,” alisema na kuongeza kuwa:
“Alishamaliza muda wake ndiyo maana tukaona ni vema tubadili damu. Tumeingiza damu mpya ili kuendana na kasi ya miradi tunayotarajia kuwa nayo.”
Bila kuhusisha kilichotokea TPA, Profesa Mukandala alisema mabadiliko hayo yamefanywa kuanzia Desemba 7, siku ambayo bodi ya TPA ilivunjwa na Rais Magufuli.
Taarifa zilizopatikana kutoka vyanzo vingine chuoni hapo vinaeleza kuwa huo ni utaratibu wa siku nyingi miongoni mwa watendaji wake waandamizi na kwamba yeyote ‘anayeharibu’ sehemu moja anakotumika akiwa mjumbe wa bodi chuo pia humwajibisha.
“Ni kanuni za chuo. Asingeweza kubaki. Mara tu baada ya Rais kuvunja bodi ya Bandari chuo nacho kilitangaza kumuondoa kwenye nafasi yake. Mtu mpya ameshapatikana na ameanza kuisimamia ofisi hiyo,” kilisema chanzo hicho. Mbali na Mgassa, wajumbe wengine waliokuwa kwenye bodi hiyo ni Naibu Spika wa Bunge, Dk Tulia Akson, Dk Francis Michael, Crescentius Magori, Flavian Kinunda, Haruna Masebu, Gema Modu na Musa Nyamsibwa.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK