Mwili wa Mtanzania Uliozuiliwa India Mpaka Walipe Deni Kuwasili Leo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Hatimaye mwili wa Mtanzania Abel Machanga aliyefia nchini India akipata matibabu unatarajiwa kuwasili leo baada ya kuzuiwa kwa takribani siku 28 kutokana na deni la matibabu.
Mwili huo umeruhusiwa baada ya familia ya Machanga kulipa deni la shilingi milioni 35 lililokuwa likidaiwa kama gharama za matibabu.

Abel alikutwa na mauti Desemba 31, 2015 akiwa kwenye matibabu nchini humo, mbaya zaidi, maiti yake ilizuiliwa kutolewa mochwari mpaka familia ilipe deni la shilingi milioni 35.
Abel alianza kuugua Novemba 2014 akiwa denti wa Chuo cha Biashara Dar (CBE). Alivimba macho, yakatokeza nje, akapoteza uwezo wa kuona huku pia akipumua kwa shida.

Alitibiwa Hospitali ya Macho CCBRT, Dar ikashindikana, akapelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili, hali ilizidi kuwa mbaya. Novemba 24, 2015, ndugu wakampeleka India ambapo mauti yalimkuta.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad