Watoto Wawili Wamshtaki Mahakamani Mchungaji TB Joshua Kwa Kifo Cha Baba yao..Wadai Fidia ya Dola $521,000

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Watoto wawili wa Afrika Kusini wanamshitaki muhubiri wa kanisa kubwa na maarufu nchinini Nigeria TB Joshua kwa kifo cha baba yao, wakili wao Bolajii Ayorinde ameiambia BBC.

Watoto hao mmoja mwenye umri wa miaka mitatu na mwingine wa miaka sita wamewasilisha nyaraka za mashtaka katika mahakama ya mji mkuu wa Nigeria, Lagos, wakidai fidia ya zaidi ya dola $521,000; kutoka kanisa la Synagogue Church of All Nations, vyombo vya habari vya Nigeria vimeripoti.

Muhubiri TB Joshua na kanisa lake wamekuwa wakisisitiza kwamba hawana kosa lolote
Baba yao alikua miongoni mwa watu 116 waliokufa wakati jengo la makazi yanayomilikiwa na kanisa hilo lilipoporomoka mjini Lagos mwaka 2014.

Mwaka jana mahakama ya uchunguzi wa vifo iliamuru TB Joshua anapaswa kushtakiwa juu ya kuporomoka kwa jengo, akisema kanisa hilo linahusika kwasababu ya uzembe wa kiuhalifu. Muhubiri TB Joshua na kanisa lake wamekua wakikana kufanya kosa lolote.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. hee huyu si anajiita nabii imekuaje tena kutupwa selo uwezo wake uko wapi? makubwa

    ReplyDelete
  2. Duh mtoto wa miaka mitatu na miaka sita? Mungu awasaidie

    ReplyDelete

Top Post Ad