AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Diwani wa Kata ya Kiwalani, Mussa Kafana (Cuf), ameibuka mshindi katika uchaguzi wa Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam, kwa kumbwaga mpinzani wake kwa kura nne.
Uchaguzi huo ulifanyika jana katika ukumbi wa Karimjee, baada ya madiwani wa jiji hilo, ambao pia ni wajumbe wa Baraza la Halmashauri ya jiji hilo kuapishwa.
Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Kaimu Mkurugenzi wa jiji hilo, Sarah Yohana alisema, Kafana ameibuka mshindi kwa kura 10 huku mpinzani wake Mariam Lulida (CCM) akipata kura sita.
“Kura zilizopigwa ni 16 na hakuna iliyoharibika. Namtangaza Mussa Kafana kuwa Naibu Meya wa Jiji la Dar es Salaam,” alisema Yohana.
Awali Meya wa jiji hilo, Isaya Mwita alisema, baraza hilo lina jukumu la kuhakikisha linatekeleza majukumu yake ipasavyo na kila mjumbe kupitia chama chake anapaswa kutoa mchango utakaoweza kulibadilisha Jiji la Dar es Salaam.
Akizungumza baada ya kutangazwa kuwa mshindi, Kafana aliwashukuru wajumbe wa baraza hilo huku akiahidi kushirikiana nao bila kubagua itikadi za vyama vyao, kwani wanafanya kazi kwa ajili ya wananchi na si vyama vyao.
Alisema kwa sasa vyama havina nafasi bali maendeleo ya wananchi wa jiji hilo ndio muhimu.
Naye Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Huduma za Sheria kutoka Ofisi ya Rais, Tamisemi, Eustard Ngate, alisema, Halmashauri ya jiji hilo ilishawahi kuvunjika mara mbili mwaka 1983 na mwaka 1996 kutokana na viongozi wake kushindwa kuwajibika hivyo hawategemei hilo litokee
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
SASA MPIGE KAZI TUONE!!!
ReplyDelete