Diamond Asema ‘WCB’ Imeajiri watu 42, Azungumzia Issue ya Kulipa Kodi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mkali wa muziki na CEO wa label ya WCB, Diamond Platnumz amesema label yake mpaka sasa tayari imeajiri watu 42.

Muimbaji huyo ambaye pia anamiliki, studio ya picha pamoja na studio ya muziki ‘Wasafi Record’, aliwaambia waandishi wa habari hivi karibuni kuwa kila anachokipata anagawana na team yake.

“Tunashukuru mungu kile tunachokipata tunagawana na wengine, mpaka sasa tayari WCB imeajiri watu 42, hii ni hatua kubwa sana katika tasnia ya muziki wetu,” alisema Diamond.

Katika hatua nyingine, Diamond amesema ni swala la kiungwana kulipa kodi katika kile anachopita.

“Unajua katika kila penye biashara ni lazima na ni haki kulipa kodi ili pato la taifa liingie, namna ya mapato maana yake nini, serikali inatambua kazi na inailinda. So serikali ipo na inafanya hivyo, lakini labda kuna nyanja nyingine hawazioni, kwa hiyo sisi kama tunataka kazi zetu zichangie pato la serikali, lazima tuwe mstari wa mbele katika kuonyesha nyanja zote za mapato, kwamba tunafanya hichi na hichi, ridhiki zetu zinatokea hapa na hapa, mishahara yetu tunagawa hivi na hivi, na kama serikali inavyoagiza katika kiasi hichi tunatakiwa kutoa kiasi hichi kwa ajili ya serikali. Kwa hiyo tusilalamike tu serikali haifanyi kazi wakati sisi tunaweza kuwa wa kwanza kuirahisishia serikali kutekeleza majukumu yake,” alisema Diamond.

 Bongo5
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hao watu 42 wenyewe ni wale wenye qualification zao????? Ama ni wale vilazaaaa???? Lipa kodi bwana mdogo.

    ReplyDelete

Top Post Ad