Wanafunzi Wafundishana Wenyewe Shule ya Kwedichocho Handeni Baada ya Walimu Kuacha Kazi.

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Wakazi wa kijiji cha Manga kilichopo kata ya Mkata wilayani Handeni wameiomba serikali kuingilia kati kufuatia walimu wawili wa shule ya msingi Kwedichocho kuacha kazi tangu mwishoni mwa jana na kuwaacha wanafunzi wakifundishwa na wanafunzi wenzao wawili wa darasa la saba kufuatia vitongoji vyao pamoja na shule kuuzwa kwa mwekezaji ikidaiwa kuwa ipo maeneo katika kijiji kingine kinachojulikana kwa jina la Mazingara.

Wakizungumza katika kijiji cha Kwedichocho baadhi ya viongozi wa serikali ya kijiji na wakazi wake wamesema hatua hiyo imekuja baada ya baadhi ya viongozi wa kijiji cha Mazingara kumuuzia mwekezaji hekari zaidi ya 400 zenye makazi ya watu zaidi ya 1000 pamoja na shule hatua ambayo wanafunzi wameanza kutishiwa kuondoka kwa sababu mwekezaji anataka kulifanyia kazi eneo la ardhi ikiwa ni pamoja na majengo ya shule pamoja na nyumba ya mwalimu.

Kwa upande wake mwenyekiti mstaafu wa kijiji hicho Saleh Sadick amesema wakazi wa vitongoji vya Kwedichocho na Mkulumilo vyote vilivyopo katika kata ya Mkata hawatakubali kuondoka katika eneo hilo linalodaiwa kuwa ni eneo la kijiji cha Mazingara hatua ambayo inaweza kusababisha uvunjifu wa amani baina ya pande hizo mbili.

ITV ilifika hadi katika shule ya msingi Kwedichocho ambapo wananfunzi walikutwa darasani wakifundishwa na wenza wa darasa la saba huku wakiimba wimbo unaosema bado mapambano yanaendelea.


----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad