AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Abdul alifanikiwa kuchukua tuzo hiyo, akimpita Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ kutoka Simba na kiungo mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Shiza Kichuya (ambaye ametua Simba), huku akichota Shilingi 9,228,820.
Abdul amesema siri kubwa za mafanikio yeye kushinda tuzo hizo ni muda mwingi alioutenga kwa ajili ya kupumzika na siyo kufanya starehe kama walivyokuwa wachezaji wengine.
Alisema sababu nyingine ni, nidhamu ya ndani na nje ya uwanja ikiwemo kutimiza majukumu yote anayopewa na kocha wake Mholanzi, Hans van Pluijm na msaidizi wake, Juma Mwambusi.
Alimalizia kwa kutaja kuwa ni kujituma kwake ndani ya uwanja kumemsaidia yeye kushinda tuzo hiyo ya uchezaji bora huku akiahidi kuendelea kupambana kwenye msimu ujao ili aichukue tena kwa mara ya pili tuzo hiyo.
“Haikuwa kazi rahisi kwangu mimi kushinda tuzo hii niliyoshinda ya uchezaji bora kwenye msimu huu, kiukweli nilijitahidi kufuata kanuni zote za mchezaji ambazo mchezaji anahitaji kuwa nazo.
“Nazo ni kupata muda mwingi wa kupumzika kwa maana ya kulala ili kupumzisha mwili mara baada ya kutoka mazoezi na siyo kwenda kufanya starehe kama ilivyokuwa kwa wachezaji.
“Nilijitambua na kutimiza majukumu yote niliyokuwa nikipewa na kocha kabla na baada ya mechi kuhakikisha ninacheza kwa kiwango cha hali ya juu, pia nidhamu yangu ilichangia kwa kiasi kikubwa,”alisema Abdul.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK