AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya shirika hilo na wadau mbalimbali wa masuala ya mafuta na gesi, zimeeleza kuwa kusimamishwa kazi kunatokana na ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu (CAG) ya mwaka jana iliyoeleza kuwa, TPDC ilikiuka taratibu za manunuzi ya umma kwa kuipa upendeleo kampuni ya Marekani kutafiti mafuta na gesi katika maeneo ya kaskazini na magharibi mwa Ziwa Tanganyika, Songosongo, Mandawa na Eyasi.
“Shirika kwa sasa si salama, kwani mkurugenzi amepewa barua kutoka kwa mwenyekiti wa bodi kusimamishwa kazi kuanzia jana (Jumatano) kutokana na ripoti ya ukaguzi,” alisema mmoja wa watoa taarifa.
Hata hivyo, mpaka jana jioni hakukuwa na taarifa rasmi kuhusu kusimamishwa kazi kwa mkurugenzi huyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa alipoulizwa kuhusu hatua hiyo, alisema anafahamu suala la kusimamishwa kazi kwa Dk Mataragio, lakini akaongeza kuwa, maelezo zaidi kuhusu maamuzi hayo anayo Mwenyekiti wa Bodi ya shirika hilo, Profesa Sufian Bukurura.
Hata hivyo, Mwenyekiti huyo alipotafutwa kwa simu kutoa taarifa rasmi za kusimamishwa kazi kwa mkurugenzi huyo, hakupatikana kwani mara zote simu yake ilisema inatumika.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK