Jeshi la polisi: Tunafanya mazoezi kupambana na uhalifu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Jeshi la Polisi kanda maalumu ya Dar es salaam, limeendelea na mazoezi yake kwaajili ya ukakamavu ili kujiweka sawa na kupambana na tatizo la uhalifu.


Akiezungumza na waandishi wa habari Kamishna wa polisi kanda ya Dar es salaam, Simon Siro, aliwatoa hofu wananchi kuwa wasiwe na wasiwasi na zoezi hilo kwani halipo kwaajili ya kuwatisha bali lengo ni kupambana na wahalifu na majambazi.

“Eeh kimsingi ni mazoezi ambayo tunayafanya kupitia maeneo mbalimbali kwa maana kwamba lengo kubwa ni kuzuia uhalifu hilo ndo lengo la kwanza, la pili ni kupambana na uhalifu kwasababu tunapokuwa tunapita maeneo mbalimbali lolote linaweza kujitokeza, wahalifu wanaweza jitokeza”, alisema kamanda Siro.

Aliongeza kwa kutoa mfano wa matukio yaliowahi kutokea alisema, “matukio mengi unaweza kuona kama ya panya rodi yanatokea sana sana maeneo ya Mbagala, lakini tukaona kwanini tufanye mazoezi haya kimya kimya ni vizuri wananchi wa kaona jeshi lao wakaona ukakamavu wa askari wao.”

“Hata miaka ya nyuma tulikuwa tunafanya na wala hatuna nia mbaya kabisa kwamba tunatisha wananchi hapana hatuna lengo la kutisha tunafanya katika mazoezi yetu ya kawaida na lengo kubwa kuzuia uharifu kwenye maeneo kwasababu naamini mtu muharifu akiona polisi anapita anakimbia”, aliongeza .

Naye kamishna wa oparesheni wa mafunzo ya jeshi la polisi Nsato Nsazya, aliwataka wananchi wasikejeli mazoezi hayo na kusema hatua kali zitachukuliwa dhidi ya watakaobainika kufanya hivyo kwa njia mbalimbali ikiwemo kupitia mitandao ya kijamii.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

6 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Sijwahi sikia wala kuona dunia nzima eti polisi wakafanya mazoezi kwenye maeneo ya raia
    Tanzania tumeendelea kweli
    Kwani hawana mafunzo vituoni
    Hongereni kwa intelinjisia bora duniani!!!!!!!!???

    ReplyDelete
  2. Mazoezi tunayoyajuwa dunia nzima ni mazoezi ya maafa, moto,
    Mafuruko , hospital nk
    Haya hufanywa kwenye maeneo ya raia
    Lakini si ya kejeshi
    Naona mna lenu Jambo
    Mungu ibariki Tanzania

    ReplyDelete
  3. Fyuuuuuuu
    Tangu lini ukamuonesha mhalifu au Adui utakavyo mkabiri
    Kwa kumuonesha silaha au njia gani utumiazo
    Kweli polisi wa bongo vilaza Kabisa

    Kwa kuwasha maji na mabomu ya machozi

    Adui akivaa musk na bullet proof utampata
    Nasikia kutapika

    ReplyDelete
  4. Siro nawe u jipu
    Bora jitumbuwe kabla hujatumbuliwa
    Kwani umekuwa msemaji wa jeshi la polisi
    Wewe ni Kamanda
    Fyuu rudi shule
    Tumekuchoka kwenye media
    Fyuuuuuuhhhhh
    Hata huyo bosi wako mkuu wa jeshi la polisi haonekani mitaandao au media Kama wewe una Fanya kazi saa ngapi
    ?
    Au unapiga doria mkuu masaa 24 ?????????

    ReplyDelete
  5. Jeshi letu ni Imara na Zuri zana. Makamand wetu na vijana wetu wako sawa kabisa katika jukumu lao la kutulinda sisi Rais na Mali zetu. Fikira na mwonekano ni Mzuri na Imetujengea Imani kwamba Amani tunayo na Itaendelea kuwepo. Sasa nyie mnaotaka kutujaribu mjue kabisa kwamba mkijaribu hatutosita kukushughulikieni. fanyeni kazi mjenge taifa na kuleta maendeleo. Ukijaribu tutacheza na wewe.. Hapa Kazi Tu. Hongera wana Usalama wetu na Majeshi yetu imara na Makachero wetu. Tunaaminini tuko katika Mikono Salama. chini ya Baba JPJM. Mungu akubarikini na kukulindeni wote na adumishe Amani na Utulivu nchini kwetu. Mungu Ibariki Tanzania na Watu wake.

    ReplyDelete
  6. Jeshi letu ni Imara na Zuri zana. Makamand wetu na vijana wetu wako sawa kabisa katika jukumu lao la kutulinda sisi Rais na Mali zetu. Fikira na mwonekano ni Mzuri na Imetujengea Imani kwamba Amani tunayo na Itaendelea kuwepo. Sasa nyie mnaotaka kutujaribu mjue kabisa kwamba mkijaribu hatutosita kukushughulikieni. fanyeni kazi mjenge taifa na kuleta maendeleo. Ukijaribu tutacheza na wewe.. Hapa Kazi Tu. Hongera wana Usalama wetu na Majeshi yetu imara na Makachero wetu. Tunaaminini tuko katika Mikono Salama. chini ya Baba JPJM. Mungu akubarikini na kukulindeni wote na adumishe Amani na Utulivu nchini kwetu. Mungu Ibariki Tanzania na Watu wake.

    ReplyDelete

Top Post Ad