Afande Aitolea Ufafanuzi Picha Aliyopiga na Makamu wa Rais Samia Baada ya Watu Kudhani Ameondoka ACT

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kitendo cha Afande Sele kupiga picha weekend hii akizungumza mbele ya Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan mkoani Morogoro, kiliibua tetesi katika mitandao ya kijamii zikidai huwenda mwanachama huyo wa ACT amekitosa chama hicho.
afande
Afande Sele akiwa mbele ya msafara wa Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan

Mwanahiphop huyo ambaye aligombea ubunge katika uchaguzi uliyopita kupitia ACT Wazalendo, wiki moja iliyopita alionyesha kutoridhishwa na mwenendo wa chama chake.

Jumamosi hii baada ya watu kuona picha hiyo na kudhani amekitosa chama cha ACT, aliandika

Aisee Watanzania sisi wengi wetu hata sijui nani katuloga kiasi cha kufunga kabisa uwezo wetu wa kufikiri nakushindwa kutofautisha hata vitu vidogo na vya kawaida sana vinavyotokea ktk maisha yetu ya kila siku…hebu tazama hiyo picha utaona mimi nipo na makamu wa rais,mkuu wa mkoa wetu na viongozi wengine wa serekali,hiyo inamaanisha kwamba hapo niliitikia wito wa serekali sio wito wa chama chochote cha siasa kitu ambacho hata viongozi au wabunge wa upinzani hufanya hivyo kwasababu serikali na viongozi wake ni mali yetu sote kama raia wa Tz sio mali ya chama fulani hata kama viongoz hao wametokana na chama hicho lkn wakishachaguliwa na wananchi wakapewa dhamana ya kuongoza tayari wanakua ni viongoz wa watu wote ktk taifa sio viongozi wa watu wa chama chao tu,sasa nashangaa pale mtu mmoja kwa sababu ya uvivu tu wakufikiri au labda kwa makusudi tu anaamua kuambukiza uvivu wake huo wa kufikiri na kutofautisha mambo kwa watu wengine…mimi nimeitikia wito wa serekali’mamlaka’ninayoamrishwa kuyatii hata ndani ya vitabu vitakatifu sio chama…lkn pia ktk hali ya kawaida tu ninani mwenye utimamu wa akili ktk taifa lolote awezae kukaidi wito wa makammu wa rais ambae ni sawa na rais wa taifa lake?lkn hata kama ingekua kweli mimi nimehama chama ingawa sifikirii kufanya hivyo bado yangebakia kuwa ni maamuzi yangu na yangepaswa kuheshimiwa…nyongeza ni kwamba hata yule mgombea urais wa marekani kupitia chama cha Republican mr donald trump siku za nyuma alikua ni mwanachama mtiifu wa chama cha mpinzani wake bibi clinton cha democratic na maisha yanaendelea..watz tujifunze maana ya maisha halisi tusijenge taifa la uzushi,fununu na kupakaziana…muwe na j’pili kareem akina ndugu nyote!
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad