Mtatiro amwambia Gavana Benki Kuu Tanzania "Mungu anakuona"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya CUF, Julius Mtatiro ameandika haya kupitia ukurasa wake wa facebook

Gavana Benno Ndulu, Mungu anakuona! Ukweli utakuweka huru, hali ya uchumi wa nchi yetu ni mbaya mno. Unapaswa kuwaeleza Watanzania ukweli huo na kushauri njia za kufuata na hatua ambazo serikali inapaswa kufanya. Kuendelea kusisitiza kuwa Uchumi wa nchi unaimarika wakati mambo kibao sana yamesimama serikalini kwa visingizio lukuki ni kujidanganya wewe mwenyewe. Ukweli na Uwazi ni moja ya siri muhimu za Uongozi imara duniani. Niwakumbushe watanzania ule msemo wa Kiganda "...President Museveni has more than 30 Economic advisers, when they convene to advise him it is him (Museveni) who advises the advisers". (Rais Museveni anao washauri wa Uchumi zaidi ya 30, na wanapokaa kumshauri ni yeye "Museveni" ndiye anawashauri hao washauri".

JSM.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. NGUVU YA SHUKRANI

    "Katika maisha yangu siwezi kusahau mchango mkubwa wa Mzee Ali Hassan Mwinyi. Mzee Mwinyi akiwa Mwenyekiti wa CCM ndiye alisimamia kikao cha Chama kilichoniteua mimi kwa mara ya kwanza kugombea Ubunge wa Jimbo la Biharamulo Mashariki mwaka 1995. Kama Mzee Mwinyi angekata jina langu siku ile, huenda leo mimi nisingekuwa hapa. Nakushuruku sana Mzee wangu Mwinyi maana huo ulikuwa ndiyo mwanzo wa safari yangu ya uongozi. Pili, ninamshukuru pia Mzee Benjamini William Mkapa ambaye aliniteua kuwa Naibu Waziri wa Ujenzi mwaka 1995 mara tu baada ya kuchaguliwa kuwa Mbunge. Mwaka 2000 akiwa Mwenyekiti wa CCM aliniteua kugombea Ubunge na nilipochaguliwa alinifanya kuwa Waziri kamili wa ujenzi hadi mwaka 2005. Nashukuru kwa kuniamini na kunipa nafasi ya kugombea Ubunge na kuniteua kwa nafasi ya Uwaziri tena bado nikiwa na umri mdogo. Mzee Mkapa ahsante sana.

    Ninamshukuru Mzee Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ambaye aliendelea kunilea katika uongozi kwa kuniteua kuwa Waziri wa Wizara mbalimbali, ikiwemo Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Wizara ya Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi pamoja na Wizara ya Ujenzi. Kwa Mzee Kikwete mbali ya kupitisha jina langu kugombea Ubunge wakati akiwa Mwenyekiti wa CCM mwaka 2010 aliamua kujitishwa mzigo, mzito wa kusimamia mchakato wote wa kumpata Mgombea Urais 2015, akaniamini hadi kuteuliwa na mikutano husika ya CCM. Kwa Mzee Kikwete pia nimejifunza mambo mengi lakini kubwa zaidi ni uvumilivu na ustamilivu. Nasema kwa dhati kabisa kuwa Mzee huyu ni mvumilivu na mstamilivu sana. Ni viongozi wachache wenye uvumilivu na ustahimilivu wa namna hii. Binafsi sina cha kumlipa zaidi ya kutoa ahadi ya kufanya kazi kwa bidii ili kumuenzi." - Rais John Pombe Magufuli (Mkutano Mkuu wa CCM, Dodoma julai 23, 2016)

    ReplyDelete

Top Post Ad