Mpenzi Mpya wa Wema Sepetu Afungukia Kwanini Alisema Hamjui Idris Sultan

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Model Calisah ambaye anadaiwa kutoka kimapenzi na Wema Sepetu amekataa kuzungumzia mahusiano yake na Wema Sepetu pamoja na kueleza kwanini alisema hamjui aliyekuwa mpenzi wa zamani wa Wema Sepetu na mshindi wa Big Brother 2014, Idris Sultan.

wema-sepetu-1

Wiki moja iliyopita kupitia kipindi kimoja cha runinga, model huyo alisema hamjui Idris Sultan.

Akiongea na Bongo5 Jumanne hii, Calisah alisema ni kweli kwamba hamjui Idris Sultan na wala hakuongea kwa nia mbaya au kutafuta kiki.

“Mimi nashangaa kwanini watu wamepanic kisa kusema simjui Idris Sultan, kwani yeye ni nani kila mtu amjue?,” aliuliza Model huyo. “Wewe kuna wanamichezo wangapi wameshachukua tuzo kubwa duniani hawajui?. Kwahiyo mimi nadhani watu ambao wananishambulia katika mitandao hawajui nini wanafanya,”

Aliongeza,”Sikusema hivyo kuonyesha dharau, kwa sababu nipo karibu na Wema lakini hajawai kuniambia kuhusu mtu kama huyo na sijawahi kumuona naye, na kama ukiwa na mwanamke halafu akawa azungumzia mwanaume mwingine hizo ni dharau sana. Kwahiyo kiukweli mimi jamaa nimeanza kumjua baada ya watu kinitag picha zake katika mitandao ya kijamii,”

Pia model huyo alisema kwa sasa hawezi kuweka wazi kama ni kweli anatoka kimapenzi na Wema Sepetu huku akidai Wema ndiye atayekuwa na jibu sahihi juu yake.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Perfect answer!!! Sio lazima kumjua mtu

    ReplyDelete
  2. Siku hizi yupo wapi yule demucwa kuitwa"MGAGAGIGIKOKO(GIGGY MONEY)Ameishiwa na mpya nini?

    ReplyDelete

Top Post Ad