CHADEMA Waibuka Mafichoni na Kulionya Jeshi la Polisi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

NAIBU Katibu Mkuu (Bara) wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Mnyika amelitaka Jeshi la Polisi kuacha kufuatilia mikutano yao ya ndani, inayoendelea sehemu mbalimbali nchini.

Mnyika alisema hayo mkoani Singida juzi akiwa kwenye moja ya mikutano ya ndani, iliyoandaliwa na Chadema kwa lengo la kuimarisha viongozi wake ngazi ya kata na wanachama ili waweze kuwafikia wananchi wa vijijini.

Naibu Katibu huyo alisema siyo jambo zuri polisi inapotumika vibaya kufuatilia mikutano ya Chadema, wakati ipo kikatiba na kuruhusiwa na serikali.

Kwa mujibu wa Mnyika, mkutano huo uliokutanisha wajumbe wa wilaya ya Ikungi, jimbo la Singida Mjini na Singida Kaskazini, ulikuwa na lengo la kuwapika viongozi wa kata ili wakaijenge Chadema imara maeneo ya vijijini.

Akizungumzia mikutano hiyo, Waziri Mkuu mstaafu wa serikali awamu ya tatu ambaye hivi sasa ni mjumbe kamati kuu ya Chadema, Fredrick Sumaye aliwataka viongozi hao wa kata kuhakikisha chama kinapata mafanikio ili hatimaye kiweze kushika dola.

Mbali ya Mnyika na Sumaye, viongozi wengine wa Chadema waliohudhuria walikuwa Mbunge Ester Matiko (Tarime Mjini), Susan Masele (Mwanza), Rose Kamili (Manyara), Jesca Kishoa (Singida) na wajumbe wengine watatu wa sekretarieti ya Chadema makao makuu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad