AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kiongozi wa zamani wa Gambia, Yahya Jammeh amekubali kuachia madaraka na amesema anaondoka nchini humo kwenda kuishi uhamishoni.
Taarifa
za kuondoka kwa kiongozi huyo aliyetawala Gambia kwa miaka 22
zimetolewa na rais anayetambuliwa na jamii ya kimataifa Adama Barrow
kupitia mtandao wake wa Twitter.
Barrow ametangaza hayo baada ya mazungumzo ya saa kadha yaliyonuiwa kumshawishi Jammeh kukubali matokeo ya uchaguzi.
Mataifa
ya Afrika Magharibi yamewatuma wanajeshi Gambia na kutishia kumuondoa
Jammeh madarakani kwa nguvu iwapo angekaidi amri ya kuachia madaraka kwa
hiari.
Barrow
amekuwa nchini Senegal kwa takriban wiki moja. Aliapishwa kuwa rais
mpya wa Gambia katika ubalozi wa Gambia mjini Dakar Alhamisi iliyopita.
Ametambuliwa na jamii ya kimataifa kama kiongozi mpya wa Gambia.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK