Hussein Machozi Afunguka Mazito...Adai Watu Wake wa Karibu Wanataka Kumpora Mke Baada ya Kushuka Kisanii

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kwa msanii au mtu maarufu, kinga pekee inayomsaidia kuendelea kuwa na heshima yake, ni kuwa na wimbo unaofanya vizuri ama kuwa na fedha.



Anapokosa hivyo, mambo hubadilika na hapo ndipo ule usemi wa Fid Q kuwa usupastaa ni mzigo wa miiba huwa na maana. Hussein Machozi anaijua hali hiyo na kupitia mitihani aliyopitia miaka miwili iliyopita, amejifunza mengi.

“Nimejifunza kuna watu wa kweli na kuna watu feki,” Machozi ameiambia Bongo5.
“Kuna watu wa kweli ambao wamekaa na mimi kwa shida mpaka sasa hivi wapo na mimi, marafiki wa kweli. Na kuna watu baadhi ambao walikuwa wapo karibu sana na mimi kipindi nipo juu, lakini kipindi ambacho nilikuwa kimya kwa muda mrefu, wameniacha mbali wamenitupa,” anasema.

“Wamenisahau,wameninyanyasa, imefikia kipindi wengine wanatongoza mpaka mke wangu. Ni kitu ambacho kinauma sana na sio kwamba mtu anamtongoza mtu hamjui, anamtongoza anajua kabisa huyu ndio future ya Hussein Machozi, yaani ndio mtu anayemtegemea. Siwasemi wengine ni mabosi walikuwa wanajifanya mabosi na vitu kama hivyo. Lakini yote tupilia mbali, ni kwamba mimi nasonga mbele na maisha naendelea na maisha yangu, nimesahau mabaya yote, nimefungua ukurasa mpya.”

Machozi ambaye kwa sasa anaishi nchini Italia amesema amenyanyuka tena na sasa yupo tayari kurudi kwenye muziki. Anatarajia kuachia kazi yake mpya iitwayo Nipe Sikuachi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad