Kajala Afunguka Kutomuona Wema Sepetu Selo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Baada ya Miss Tanzania 2006/07 ambaye ni Mwigizaji wa Bongo Muvi, Wema Isaac Sepetu kusota lupango kwa siku kadhaa kufuatia kutajwa kwenye tuhuma za madawa ya kulevya na Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda, kabla ya kupandishwa mahakamani na kuachiwa kwa dhamana, staa mwenzake, Kajala Masanja ameibuka na kufunguka sababu ya kutokwenda kumuona mahabusu.


  Kajala, akiwa ni rafiki wa Wema, aliwahi kuokolewa kwenda jela na mrembo huyo baada ya kumlipia faini ya shilingi milioni 13, anadaiwa kutofika lupango katika Kituo Kikuu cha Polisi ‘Central’ jijini Dar alikokuwa ameshikiliwa Wema, jambo ambalo liliwashangaza wengi. Chanzo makini kililieleza Wikienda kuwa, kitendo cha kutokwenda kumuona wala kufika mahakamani siku aliyopandishwa kizimbani, kilimuumiza Wema na ndugu zake kwani hawakutegemea mtu kama Kajala angeshindwa kufika kumuona na kumsapoti shosti wake huyo.


Katika mitandao ya kijamii, gumzo lilikuwa ni Kajala kutokwenda selo kumuona Wema hadi akatoka huku watu wengine wakimporomoshea matusi.

Katika kuujua ukweli na sababu za kutokwenda kumuona rafiki yake huyo, Wikienda lilimtafuta Kajala ambapo alikuwa na haya ya kusema:

“Nimeshazoea kutukanwa bila sababu lakini mimi sikuwepo, nilisafiri ndiyo maana sikwenda na nimeumia sana kutokwenda.”

Wema ni miongoni mwa mastaa na watu mbalimbali waliotajwa hivi karibuni na Makonda wakituhumiwa kujihusisha na madawa ya kulevya ambapo Jumatano iliyopita alipandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu pamoja na dada wawili wa kazi ambapo walitoka kwa dhamana ya shilingi milioni tano kila mmoja.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. mnafiki Kajala. alirudi kabla Wema hajatoka jela.

    ReplyDelete
  2. muongo mkubwa! alirudi na wolper na le kunukazz. na alikuwa hapa hapa dar.

    ReplyDelete
  3. kajala na Makonda walishakuwa wapenzi, unafikiri ataenda kumuona Wema!

    ReplyDelete

Top Post Ad