AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kajala, akiwa ni rafiki wa Wema, aliwahi kuokolewa kwenda jela na mrembo huyo baada ya kumlipia faini ya shilingi milioni 13, anadaiwa kutofika lupango katika Kituo Kikuu cha Polisi ‘Central’ jijini Dar alikokuwa ameshikiliwa Wema, jambo ambalo liliwashangaza wengi. Chanzo makini kililieleza Wikienda kuwa, kitendo cha kutokwenda kumuona wala kufika mahakamani siku aliyopandishwa kizimbani, kilimuumiza Wema na ndugu zake kwani hawakutegemea mtu kama Kajala angeshindwa kufika kumuona na kumsapoti shosti wake huyo.
Katika mitandao ya kijamii, gumzo lilikuwa ni Kajala kutokwenda selo kumuona Wema hadi akatoka huku watu wengine wakimporomoshea matusi.
Katika kuujua ukweli na sababu za kutokwenda kumuona rafiki yake huyo, Wikienda lilimtafuta Kajala ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Nimeshazoea kutukanwa bila sababu lakini mimi sikuwepo, nilisafiri ndiyo maana sikwenda na nimeumia sana kutokwenda.”
Wema ni miongoni mwa mastaa na watu mbalimbali waliotajwa hivi karibuni na Makonda wakituhumiwa kujihusisha na madawa ya kulevya ambapo Jumatano iliyopita alipandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu pamoja na dada wawili wa kazi ambapo walitoka kwa dhamana ya shilingi milioni tano kila mmoja.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
mnafiki Kajala. alirudi kabla Wema hajatoka jela.
ReplyDeletemuongo mkubwa! alirudi na wolper na le kunukazz. na alikuwa hapa hapa dar.
ReplyDeletekajala na Makonda walishakuwa wapenzi, unafikiri ataenda kumuona Wema!
ReplyDelete