Bond Afunguka Kukamatwa Kwake...!!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Bond Bin Suleiman, amefungukia kukamatwa kwake kwenye ishu ya ujambazi na kudai kuwa aliponzwa na rafi ki yake aliyekuwa hafahamu anajishughulisha na kazi gani.

Akizungumza na Wikienda, Bond alisema kuwa, yeye ni msanii na anakutana na watu wengi kama ilivyo kwa wasanii na kilichomkuta kinaweza kumkuta msanii yeyote kwani hukutana na watu wa aina zote hasa kwenye mambo ya starehe.

“Unajua mtu akikuita akakuambia twende tukanywe au njoo nikupe ofa si rahisi kuichunguza kazi yake na kama unavyojua watu hawa hufi cha sana mambo yao.

Huyo jamaa anayetajwa alikuwa ni mtu wa kuniita na kunipa kinywaji na si mara kwa mara lakini nashangaa watu wanavyoongea kuhusiana na jambo hilo zito ambalo likimkuta mtu yeyote si rahisi kulimaliza lakini nashukuru sina kesi ya kujibu na mambo yameisha, Watanzania wajue tu sijawahi kuwa mtu wa kazi hiyo ya ujambazi,” alisema Bond.

Bond alilishukuru Jeshi la Polisi kwa kufanya kazi yao kikamilifu na kuamua kumuachia kwani haikuwa kesi rahisi na imeharibu sifa yake.

Kwa upande wa Wastara ambaye ni mpenzi wake alisema kuwa haogopi maneno ya watu kwani wanaongea sana lakini ukweli upo polisi na kama kungekuwa na kitu kama hicho, Bond asingeachiwa kirahisi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad