AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mfanyabiashara na muagizaji wa pombe za viroba, Festo Mselia, amekutwa amejiua kwa kujipiga risasi ikiwa ni siku moja baada ya jeshi la polisi kuendesha msako na kukamata shehena ya pombe katika ghala alililokuwa akilimiki mjini Dodoma.
Katika vita ya kupambana na matumizi ya pombe za vifungashio aina ya viroba vilivyopigwa marufuku, jeshi la polisi mkoa wa Dodoma limefanikiwa kukamata shehena hiyo ya katoni 1,400 ikiwa na thamani ya shilingi bilioni moja katika ghala la mfanyabiashara huyo.
Mfanyabiashara huyo aliyejiua ni wakala mkuu wa uagizaji na usambazaji wa pombe hizo akiwa anamiliki 'store' ya Mselia Intapreses.
Awali katika msako huo ulioongozwa na kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa, alimtaka mfanyabiashara huyo kuendelea na shughuli zake, huku akiamuru shehena hiyo isiuzwe wala kutumika wakati akisubiri maelekezo mengine.
Mambosasa amesema jeshi linaendelea na uchunguzi kabla ua kutoa taarifa rasmi.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK