Kashfa Faru John Kuwasomba Vigogo Wawili..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


KAMATI iliyoundwa kuchunguza utaratibu uliotumika kumhamisha Faru John kutoka Hifadhi ya Ngorongoro kwenda Sasakwa Black Rhino Sanctuary iliyoko kwenye Hifadhi ya Grumeti Serengeti, imependekeza hatua za kinidhamu dhidi ya maofisa wawili wa serikali.

Kamati haikufafanua aina ya hatua ambazo zinapaswa kuchukuliwa kwa maofisa hao, lakini umakini uliopo katika serikali ya awamu ya tano unaashiria upo uwezekano mkubwa kwa maofisa hao kutumbuliwa.

Ingawa kamati hiyo iligundua kuwa Faru John alikufa kifo cha asili, imependekeza hatua za kinidhamu kwa sababu hakukuwa na kibali rasmi cha kumhamisha kwenda mazingira ambayo yalisababisha kifo chake.

Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyelle alitoa pendekezo hilo jana wakati akikabidhi ripoti hiyo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa juu ya uchunguzi walioufanya kuhusu uhamishwaji na kifo cha mnyama Faru John.

Kamati hiyo imependekeza hatua za kinidhamu zichukuliwe dhidi ya Mkurugenzi wa Wanyamapori wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), Profesa Alexander Songorwa na Daktari wa Shirika la Hifadhi la Taifa (Tanapa), Dk. Moris Kileo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad