TFF hali si shwari’, Mgogoro wafukuta

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Hali si shwari ndani ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kumebainika kuwa mgogoro baina ya watendaji wa shirikisho hilo.


Habari za ndani zinaeleza, rais wa TFF, Jamal Malinzi amewekwa kiti moto baada ya kudaiwa kuwabadilisha watia saini wa benki huku Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ikianza kuwahoji baadhi ya viongozi wa shirikisho hilo.


Ingawa Takukuru haikuwa tayari kulizungumzia suala hilo, lakini habari zaidi zinasema viongozi kadhaa wa TFF wamehojiwa na Taasisi hiyo wakihusishwa na matumizi mabaya ya fedha za shirikisho hilo.


Mbali na Takukuru, pia imeelezwa kuwepo kwa maelewano mabaya baina ya viongozi wa Kamati ya Utendaji ya TFF huku kikao cha Machi 26 kikipangwa kutumika kumuhoji Malinzi juu ya madai ya kughushi muhtasari na kubadili watia saini.


Baadhi ya wajumbe katika kikao hicho wameeleza kutojua ajenda ingawa tayari wamepokea barua za wito wa kikao.


Ofisa Habari wa TFF, Alfred Lucas ilisema jana kuwa kikao kitafanyika Dar es Salaam na ajenda kuu itakuwa kupanga tarehe ya uchaguzi mkuu wa shirikisho utakaofanyika baadaye Oktoba.


“Wataanza kufungua kikao, kisha mengineyo na baadaye kufunga kikao, masuala mengine yanayosemwa ni siasa hakuna chochote,” alisema Lucas.


Makamu wa rais wa TFF, Walence Karia alikiri kupewa taarifa za kikao, lakini akasisitiza masuala mengine aulizwe katibu mkuu, Celestine Mwesigwa.


“Habari za kughushi muhtasari na kubadili watia saini wa benki mimi siwezi kulizungumzia, hilo ni suala la Katibu Mkuu kwanza silifahamu,” alisema Karia kwa kifupi.


Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwesigwa alipotafuwa alisema yuko na majukumu mengine hawezi kuzungumza chochote.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad