Utafiti..Wanaume Wengi Hawafahamu Ukubwa Sahihi wa Maumbile Yao..

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Moja ya jambo ambalo huwaumiza kichwa wanaume wengi ni kuwa na maumbile madogo ya kiume. Wengi huamini uume mrefu na mpana ndiyo urijali wenyewe kuweza kumfikisha kileleni mwanamke.

Wanasayansi wengi wa tiba wametoa machapisho mengi ya kitafiti kuhusu urefu na upana wa uume juu ya wastani unaokubalika.
Baadhi ya wanaume wamekuwa wakiishi kwa hofu na kukosa kujiamini katika mahusiano yao kwa kuhisi wana uume mdogo usioweza kumridhisha mwenza.

Hofu hiyo inawezekana ni kutokuwa na ufahamu sahihi juu ya maumbile yao yanavyotakiwa kuwa. Wengi wanakosa taarifa sahihi kutoka kwa wataalam wa afya wenye uelewa wa kutosha wa jambo hili.

Hofu ya wanaume inapanda zaidi kila siku hasa kutokana na utitiri wa matangazo ya magazeti, mitandaoni, stori za vijiweni na matangazo ya matabibu wa mtaani wanaojitangaza kuwa na dawa na vifaatiba vya kukuza uume.

Dondoo zifuatazo zinajumuisha machapisho ya kitafiti yakiwamo yaliyochapishwa katika majarida makubwa na maarufu duniani kama vile Science Today, Men’s Health na British Journal of Urology International.

Asilimia 85 ya wanawake wanaridhika na urefu na upana wa maumbile ya uume wa wenza wao ingawa wanaume wenyewe hawana uhakika wa jambo hilo huku asilimia 45 ya wanaume wanaamini wana maumbile madogo.

Utafiti unahitimisha kuwa wastani wa urefu wa uume ukiwa tepetepe yaani kabla ya kusimama ni kati ya sentimita saba mpaka 10 au inchi 2.8 hadi 3.9. urefu huu unapimwa kuanzia kwenye shina la uume mpaka kichwani.

Urefu wa uume unapokuwa umesimama ni kati ya sentimita 12 na16 au ichi 4.7 hadi 6.3. Urefu wa mzunguko wa uume ukiwa umesimama ni kati ya sentimita 12 au inch 4.7.

Dondoo nyingine zinaonyesha wanaume wenye unene uliopitiliza na wenye umri mkubwa wengi wao wana urefu mfupi wa uume ukiwa umesimama.

Maumbile ya uume yanatofautina kati ya jamii moja na nyingine, bara moja na jingine. Wanaume wanaotokea Asia wana maumbile madogo ya uume ukilinganisha na wanaume wa Afrika.

Wanawake wengi huwa hawajali urefu na upana wa uume wa wenza wao pengine kutokana na ukweli kuwa kufika kilele cha tendo kwa wanaweka si lazima kumuingilia, wanaweza kufanya hivyo hata kwa kutomaswa tu au njia nyinginezo.

Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake, Ernst Grafenberg wa Ujerumani aligundua sehemu muhimu inayoelezwa kuwa na msisimko wa kipekee kuliko nyingine yoyote katika sehemu za kike.

Sehemu hiyo ijulikanayo kama G-spot ambayo ipo sentimeta 5.1-7.9 au nchi 2-3 tu kuanzia nje ya uke kuingia ndani. Inaelezwa, unaweza kuwa na uume mdogo lakini ukamridhisha mwenza wako na kumfikisha kileleni ukiweza kuisisimua sehemu hiyo.

Wanaohisi kuwa na maumbile madogo wasikimbilie dawa za mtaani kwani utapeli ni mwingi bali waende kwa watoa huduma za kisasi za afya zinazotambulika kwa ajili ya ushauri..

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad