Baada ya Dakika 90 Wachezaji wa Bayern Munich Wavamia Chumba cha Muamuzi, Polisi Waingilia

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Katika kile kinachoonekana kutoridhishwa na maamuzi ya refa wa mchezo kati ya Real Madrid dhidi ya Bayern Munich Victor Kassai, baadhi ya wachezaji wakiongozwa na mshambuliaji wa timu hiyo Roberto Lewandoski walivamia vyumba vya kubadilishia nguo waamuzi baada ya mchezo huo.

Taarifa zinasema Artulo Vidal, Thiago Alcantara nao walikuwepo kwenye kikundi hicho cha wachezaji wa Bayern ambao waliingia katika vyumba hivyo vya kubadilishia nguo waamuzi kabla ya polisi kuitwa na kuwalazimisha kuondoka kwa nguvu katika vyumba hivyo.

Kipigo cha bao 4 kwa 2 katika uwanja wa Santiago Bernabeu kiliwafanya Bayern Muinch kufungasha kilicho chao katika michuano hiyo na kurudi kwao Ujerumani lakini kadi nyekundu aliyopata Artulo Vidal na goli lilioonekana la offside alilofunga Ronald liliwafanga Bayern Munich wakasirike sana.

Inasemekana wachezaji hao watatu wlivamia ofisi hizo na kuanza kumtukana muamuzi huyo huku Vidal akienda mbali zaidi kwa kumsogelea, wakati wakiendelea kufanya hivyo muamuzi aliwaomba waondoke chumba hicho lakini wachezaji hao walikataa na kuendelea kumtupia maneno yeye na wenzake.

Kitendo walichofanya nyota hao kinaweza kuwaingiza matatani kwani vhama cha soka barani humo UEFA kinaweza kuchunguza tukio hilo na ikibainika walitenda kosa baasi adhabu itawahusu.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad