Mkanganyiko Baada ya Roho Kuachana na Mwili,Roho Huenda Wapi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Haya mambo bado yanachanganya wengi kwamba roho inaenda wapi baada ya kuachana na mwili
1.Je inaenda kuzimu?
2.Je inaenda peponi? 
3.Je inazaliwa upya?
4.Je inawayawaya na kutangatanga huku na kule?

Maswali yote hapo juu yana majibu yanayofanana, kuwa roho zipo na zinakuwa kote huko kulikotajwa kutegemeana na kwenye uhai wake kidunia zilibeba/ zilifanya nini? Hebu twende moja baada ya jingine.

Kwanza, dini zote zinahimiza matendo mema na maisha baada ya kifo; hata wapagani pia. Hivyo basi, japokuwa maelezo yanatofautiana, lakini msingi unabaki kuwa ule ule wa roho kuwa sehemu husika.

1.Je, roho inaenda kuzimu? Jibu ni ndio

Kwamba bila kujali unaamini nini lakini jehanam iko hapahapa duniani , roho iliyotenda mabaya duniani baada ya kutoka katika mwili uharibikao huingia kwenye mwili mwingine uliojaa mateso tabu na mahangaiko mengi! Kumbuka ili roho iweze kubeba hisia za mateso na maumivu lazima zipate jumba/ mwili!! Hiyo ni jehanam au kuzimu.

2.Je, roho huenda peponi? Jibu ni ndio

Pepo iko hapahapa duniani, roho iliyoishi kwa kutenda mema hubaki mahali kwenye dunia hii ikiwa iko live lakini domant ikiwa haihisi wala kufanya chochote na kama ikibidi kupata mwili huingia kwenye mwili ambao haujui shida za dunia hii kila kitu kwake ni mteremko tu mpaka mwili husika unapochoka na kuharibika/ kufa!! Hii ni peponi.

3.Je, roho inazaliwa upya? Jibu ni ndio japo kimsingi sio kuzaliwa upya bali ni kupata makao/ makazi mapya hapa ndio penye dhana nzima ya reincarnation, ambapo sasa hutegemea matendo ya nyuma Kwahiyo yaweza kuwa kwenye mwili mzuri au mbaya refer pepo na kuzimu.

4.Je, roho zinatangatanga? Jibu ni ndio
kwanza roho huwa hazifi bali kuna wakati hukosa makao mapya/mwili baada ya zamani kwisha na kuharibika 
Haijulikani hasa nini hutokea lakini hizi ni roho zenye matatizo makubwa na ndio hizi huwa mashetani majini vinyamkera na viumbe vya ajabu ajabu. Ni roho hizi hizi ambazo huweza kuingia kwenye familia kikundi au mkusanyiko wowote na kuleta mirafaruku mikubwa tu ambayo mingine huleta maafa makubwa. 

Kwahiyo roho zipo na zipo sana na kamwe hazifi wala hazipotei jehanam, na pepo zao zipo hapahapa duniani na kwenye kila nyanja ya maisha yetu 
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad