AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Rais Donald Trump wa Marekani ametuma salamu za pongezi Tanzania kwa kuadhimisha mwaka wa 53 wa Muungano.
Katika salamu zilizotolewa jana jioni na kuwekwa katika tovuti ya Wizara ya Mambo ya Nje, Trump ameeleza uhusiano baina ya Tanzania na Marekani na matumaini yake ya kuuendeleza.
“Kwa niaba ya Rais Trump na wananchi wa Marekani, nawapongeza wananchi wa Tanzania wakati mnaposherehekea mwaka wa 53 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” anasema Rex W. Tillerson, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani.
“Tanzania na Marekani zina uhusiano mkubwa, unaoonyeshwa na juhudi za pamoja kufikia malengo yetu na ushirikiano wa karibu katika programu na jitihada mbalimbali, kuanzia katika afya na elimu, kuendeleza ukuaji uchumi na uongozi wa kidemokrasia na kukuza usalama wa kanda. Katika mwaka unaokuja, tunategemea kufanikisha malengo yetu ya pamoja kadri tunavyoendeleza juhudi zetu.
“Wakati Watanzania wakisherehekea Siku ya Muungano, naungana nao katika matumaini ya kuwa na amani, afya, na ufanisi.”
Hizi ni salamu za kwanza kwa Trump na Serikali yake kwa Tanzania tangu kiongozi huyo kutoka chama cha Republican asimikwe kuwa Rais wa taifa hilo kubwa duniani Januari 20 baada ya kushinda katika uchaguzi uliofanyika mwaka jana.
Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.
Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA
Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK