DAR: Yericko Nyerere Akamatwa Akiwa Nyumbani Kwake. Wachukua Simu na Laptop

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Watu waliojitambulisha kuwa ni Polisi kitengo cha cyber crime! Wamefika mda huu majira ya saa 7:04 usiku, Kwa Yericko Nyerere wakiambatana na mwenyekiti Wa mtaa (Mbutu), walipofika wamemchukua yeye pamoja na vifaa vyake ikiwemo simu na laptop yake na kuondoka naye kuelekea kituo cha police kigamboni wakimtuhumu kuhusika na kosa la kimtandao.(ingawa hawakueleza kosa halisi kafanya lini na wapi).

Taarifa zaidi mtaendelea kuzipata baadae.
Ikumbukwe hii ni Mara ya pili kukamatwa kwake, baada ya kesi yake iliyodumu Kwa miaka miwili tangu kipindi cha uchaguzi ambapo alishinda na kuachiwa huru mapema April 2017.



UPDATES:

Taarifa zilizonifikia hivi punde nikwamba; kituo cha kigamboni hakija mshikilia Yericko, na wala hawajui alikamatwa Kwa kosa gani; kutokana na taratibu za kazi wao kama polisi.

Wenyeji walitoa ushirikiano kutokana na jiografia ya eneo analoishi Yericko kuwa ni porini pembezoni mwa mji, kiasi kwamba Kwa gari yao (oppa) waliokuja nayo, isingekuwa rahisi kufika, Kigamboni waliombwa msaada wa gari (Defender) ili kuweza kufika eneo husika, na walipomkamata walimpekua, na baadaye kuondoka naye Kwa gari yao kuelekea makao makuu!

Kigamboni Polisi hayupo na wala hakufikishwa, walimchukua juu Kwa juu kwenye gari yao nakuondoka naye.

"Askari Wa Doria kigamboni alijaribu kuwahoji wale jamaa kutaka kujua mtuhumiwa ana kosa gani, jamaa walimjibu Kwa mkato " AMEPIGA PALEFU"

Taarifa zaidi mtajuzwa baadae! Kama kuna mtu yeyote anaweza kujitokeza Kwa mambo ya dhamana na taratibu za kisheria mnakaribishwa tukutane pale makao!
-----

New Updates..

Kwa mujibu wa Malisa G; Yericko Nyerere alipokamatwa usiku wa saa 5, alilazwa ktk kituo cha Polisi Kigamboni na asubuhi hii amehamishiwa Central(Dar) ambapo viongozi wa CHADEMA watawasili kudai maelezo ya sababu za kukamatwa kwake.


Source:Jamii Forums
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad