AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete jana usiku amekutana na nahodha wa Timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Mbwana Samatta huko Ubelgiji alikoenda kwa ajili ya Mkutano wa kutatua migogoro ya kisiasa nchini Libya.
Mzee Kikwete mapema baada ya kukutana na nyota huyo anayekipiga kunako Klabu ya Genk alionesha furaha yake na kuandika ujumbe mzuri wa kufurahishwa kwa kukutana nae.
“Nikiwa hapa Brussels kuhudhuria Mkutano wa Wadau wa Libya nimepata fursa ya kukutana na mwanasoka na kipenzi chetu @samatta77 leo hii“, Ameandika Kikwete lwenye ukurasa wake wa Twitter.
Samatta nae hakuchukulia poa shavu hilo la kutembelewa na Rais Mstaafu kwa Kuandika “Ni wakati mzuri siku zote kukutana na our former president Mr @JakayaKikwete Wise and charming man. Asante sana mheshimiwa mungu akuweke” .
Mbwana Samatta ni moja ya wachezaji ambao wametajwa kwenye kikosi cha Taifa Stars kinachojiandaa kuvaana na Lesotho mwezi ujao kwenye mechi za kufuzu AFCON.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK