MAGUFULI Ampa Tano Dk Mengi kwa Uwekezaji Nchini..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


RAIS John Magufuli amempongeza Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP, Dk. Regnald Mengi kwa kufanya uwekezaji wa Kiwanda cha Kutengeneza Vinywaji Baridi Jamii ya Coca Cola cha Bonite Bottlers Limited (BBL) cha Moshi mkoani Kilimanjaro.

“Nimemuona Dk. Mengi yuko pale na kwa kweli naomba nimpongeze kwa kile Kiwanda chake cha Bonite alivyowekeza, hongera sana. Wazawa wengine wa Kilimanjaro rudini nyumbani muwekeze. Huyu Dk. Mengi anapiga kote kote Dar na Moshi,”alisema.

Rais Magufuli alitoa pongezi hizo  wakati wa sherehe za maadhimisho ya sikukuu ya wafanyakazi duniani (Mei mosi) zilizofanyika kitaifa mjini Moshi kwenye viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi.

Pongezi hizo za Rais, ziliamsha hisia za furaha za maelfu ya wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro waliofurika katika sherehe hizo na kumshangilia Dk. Mengi, baada ya Rais Magufuli kumsimamisha na kumtaka awapungie mkono.

Dk. Mengi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) amekuwa akisisitiza suala la uwezeshaji wananchi kiuchumi kuwa ni njia pekee duniani iliyoonesha mafanikio katika kukuza uchumi wa nchi mbalimbali,kupunguza umaskini na kudumisha amani na utulivu.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad