SHULE Ambayo Wanafunzi Wake Wamefariki kwa Ajali ya Basi Arusha Yafungwa kwa Wiki Moja..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Shule ya Lucky Vicent imefungwa kwa siku saba kufuatia vifo vya wanafunzi wake 32 vilivyotokea kwenye ajali ya gari jana Karatu.

Kutokana na ajali hiyo Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema na wabunge wengine wa Chadema wamefika shuleni hapo kutoa pole.

Lema kwa niaba wabunge ameeleza kusikitishwa na msiba huu na amewapa pole wafiwa lakini akatoa angalizo kusiingizwe siasa katika msiba huu mkubwa.

Meya wa jiji la Arusha Kalist Lazaro ameeleza kuwa Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, Waziri wa Tamisemi, George Simbachawene na Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako watafika jioni kuzungumza na wafiwa.

Leo Makamu wa Rais Samia Suluhu kwa niaba ya Rais John Magufuli ataongoza kazi kuaga miili ya wanafunzi hao Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.

Mkuu wa shule hiyo, Ephraem Jackson amesema  hadi sasa vifo ni 36 na wanafunzi wawili bado wamelazwa Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru. Wanafunzi hao ni Sadiely Ismail na Wilson Tarimo.

----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad