STEVE Nyerere Majanga Tena

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

Baada ya hivi karibuni nyumba yake kuvamiwa na kunyofolewa madirisha, msanii wa vichekesho Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ amepata majanga tena kufuatia mwanaye kupotea katika mazingira ya kutatanisha.

Chanzo kilieleza kuwa motto huyo alitoweka nyumbani kwao, Kinondoni Mkwajuni, Dar siku tatu zilizopita na kumsababisha Steve kuwa na wasiwasi mkubwa kwamba huenda ametekwa au la kwani amejaribu kutafuta kila sehemu bila mafanikio.

“Yaani mwaka huu Steve ana majanga makubwa maana hata hajapumzika na tukio la kuibiwa, limetokea tena hili la kupotelewa na mwanaye ambaye ni mwanafunzi yaani ana haha kweli,” kilisema chanzo.

 Baada ya kupata habari hizo, Amani lilimtafuta Steve ambaye alikiri kupotelewa na mwanaye anayejulikana kwa jina la Linda Raymond (17) ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha nne kwenye shule moja iliyopo wilayani Moshi, mkoani Kilimanjaro.

“Siku ya tukio ambayo ni Jumapili saa kumi na mbili jioni mwanangu alitoweka nyumbani kwangu Kinondoni Mkwajuni na nimejaribu kumtafuta kila kona lakini sijafanikiwa ambapo tulienda polisi na kufungua kesi kwa jalada OB/RB/697110/17.

“Nawaomba Watanzania wanisaidie jamani popote watakapomuona watoe taarifa kituo chochote cha polisi kwani ni mwanafunzi wa kidato cha nne halafu nimejaribu kwenda kuangalia kwenye mtandao wa simu mtu wa mwisho kuwasiliana naye inaonekana ni mwanaume amemtorosha, hatujui ni kwa lengo gani maana sasa hivi hofu kubwa isiwe ametekwa,” alisema Steve.
NA GLADNESS MALLYA
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad