TRAFIKI Wakusanya Milioni 400/- kwa Siku 5...!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


JESHI la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limekusanya zaidi ya Sh milioni 400 kwa siku tano, baada ya kukamata magari na pikipiki zilizofanya makosa 13,584 barabarani.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, Simon Sirro, alisema kuanzia Mei 9 hadi 14, kikosi hicho kilifanya ukamataji wa makosa mbalimbali ya barabarani na kukusanya kiasi hicho cha fedha.

“Idadi ya magari yaliyokamatwa ni 11,174, pikipiki 643, daladala 4,902, magari mengine (binafsi na malori) 4,376 na bodaboda waliofikishwa mahakamani kwa kutovaa kofia ngumu na kupakia mishikaki ni sita,” alisema Sirro.

Pia, Jeshi la Polisi Kanda hiyo lilitoa taarifa za kuuawa kwa jambazi kwa kupigwa risasi Kurasini katika jengo la Makao Makuu ya Uhamiaji ambaye alijaribu kumnyang’anya silaha askari aliyekuwa akisindikiza gari la kampuni ya G4S lililokuwa limebeba Sh milioni 320 zilizokuwa zikisambazwa kwenye ATM za benki ya CRDB.

Akizungumzia kuuawa kwa jambazi, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 9.50 alasiri na fedha hizo zilikuwa kwenye gari namba T 155 DGB aina ya Nissan mali ya G4S huku likisindikizwa na askari wawili wa FFU ambao walikuwa kwenye gari namba T 997 DGQ mali ya kampuni hiyo pia.

Alieleza kuwa katika eneo hilo,  kulikuwa na watu wanne kwenye pikipiki mbili aina ya Boxer ambazo hazikusomeka namba na wakati wahudumu wa gari hilo wakisambaza fedha kwenye ATM, ghafla mmoja kati ya watu wale aliruka na kumvamia askari Konstebo Adam kwa lengo la kumpora silaha ili kufanikisha uporaji.

Alibainisha, kwamba baada ya kitendo hicho jambazi huyo aliamriwa kusimama lakini alikaidi na ndipo akapigwa risasi iliyomjeruhi mguuni na nyingine tumboni na kuishiwa nguvu na kuwekwa chini ya ulinzi. Majeruhi alifariki dunia akiwa njiani kupelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).

Aidha Kamishna Sirro alisema msako unaendelea wa kukamata watuhumiwa wengine waliokimbia na pikipiki.

Kwa upande mwingine Jeshi hilo linashikilia watuhumiwa 120 kwa makosa mbalimbali ya kihalifu ikiwa ni pamoja na dawa za kulevya kutokana na msako uliofanyika kuanzia Mei 9 hadi 14.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad