WANAFUNZI wa Lucky Vicent Wafunguka Haya Mazito Baada ya Wenzao 33 Kufariki Katika Ajali ya Basi Juzi..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Baada ya Shule ya Msingi ya Lucky Vicent kupoteza wanafunzi 32, walimu wawili na dereva katika ajali ya gari iliyotokea wilayani Karatu, wanafunzi wengine wamesema wamebaki nusu ya wanafunzi bwenini.

Kila mwanafunzi ameonekana mwenye hisia katika hafla maalumu ya kuaga miili ya wenzao kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini hapa na msiba huu unaonekana utaendelea kuwa katika vichwa vya wanafunzi waliobaki kwa muda mrefu.

Ndiyo maana imemlazimu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk Eva Maria Semakafu kutoa ushauri wa uongozi wa elimu jijini Arusha, kuwatafutia mwalimu wa saikolojia ili awawezeshe kukabiliana na hali hiyo.

Noreen Josia, mwanafunzi wa shule hiyo anayesoma darasa la sita, anasema hatasahau msiba huo.

Anasema alishtushwa na taarifa kuwa gari lao la shule limepata ajali kutokana na simu ambazo zilikuwa zinapigwa na pia taarifa kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.

“Nilirudi shuleni kuuliza kama ni kweli, nikaambiwa ni kweli. Tangu wakati huo hadi sasa, sijisikii vizuri, nahisi kuumwa kwa kuwa bwenini kwetu karibu nusu ya wanafunzi sijawaona. Nadhani wamefariki,” amesema huku akitokwa na machozi.

Noreen, ambaye muda mwingi, alikuwa ameshikiliwa na watoa huduma wa Msalaba Mwekundu, alisema: “Siwezi kusahau kwa kuwa tulikuwa nao bwenini wakati wakijiandaa kwenda kwenye mitihani ya majaribio Karatu na tuliagana. Sasa kuambiwa hawapo tena ni jambo ambalo siwezi kusahau,” anasema.

Noreen anawakilisha idadi kubwa ya wanafunzi wa shule hiyo ambao wameathiriwa na msiba huo mkubwa wa aina yake na ambao wamepewa siku saba za mapumziko kwa majili ya kutuliza akili.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Ephraim Jackson anasema, wanafunzi 96 wa darasa la saba ndio walisafiri kati ya wanafunzi 106 wa darasa hilo.
----

Love Story ya NJIA PANDA,Ni Kali mnoo Jamani.

Kusikiliza au kusoma mwendelezo wake Tembelea www.makapedia.com kisha bofya palipoandikwa NJIA PANDA kila siku saa moja kamili jioni BURE au bofya HAPA

Pia Bofya HAPA kujiunga na what's app channel yetu,tukukumbushe kila siku.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad